BANDA MEDIA BLOG

CLUB YA WAANDISHI WA HABARI DODOMA YAFANYA MKUTANO WAKE MKUU WA MWAKA, HUKU WAKIELEKEZA LAWAMA KITENGO CHA HABARI OFISI YA MKUU WA MKOA

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini Christina Mndeme akizungumza jambo wakati alipokuwa akifungua mkutano mkuu wa Club ya Waandishi wa Habari wa mkoa wa Dodoma, kulia ni Mwenyekiti wa Club hiyo Habal Chidawali na kushoto ni Katibu Bilson Vedastus

Waandishi wa habari wakiwa katika mkutano huo


Waandishi na Wadau wa habari wakifuatilia mkutano, PICHA ZOTE NA JOHN BANDA



Mwandishi wa Tanzania Daima Hamida Ramadhan akichangia jambo katika mkutano huo

picha ya pamoja na mgeni Rasmi
Na John Banda, Dodoma
WAANDISHI wa habari mkoani Dodoma wamesema kutokana na kutopata ushirikiano katika kitengo cha Habari na mawasiliano cha ofisi ya mkuu wa mkoa huo kinawanyima wakazi wake na watanzania kwa ujumla haki ya kupata habari ambayo ni haki yao kikatiba.
Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Clabu ya Waandishi wa habari mkoani Dodoma [CPC] Wakati wa mkutano wake mkuu wa mwaka uliofanyika juzi katika ukumbu wa New Dodoma Hotel ambapo Mgeni Rasmi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini Christina Mndeme kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Jordan Rugimbana
Mwenyekiti huyo alisema hakuna ushirikiano kwa muda mrefu sana kati ya waandishi wa habari wa mkoa huo na kitengo cha habari cha ofisi ya mkuu wa mkoa na hata wanapojaribu kuyatengeneza wao wanagonga ukuta
Alisema pamoja na jitihada walizowahi kufanya hazikufanikiwa kwa mhusika/ wahusika wa kitengo hicho mara zote wapo bize na mambo yao huku wakisahau kuwa habari ni haki ya wanadodoma na watanzania kwa ujumla
“nitakuwa sijawatendea haki kama sitaanza na changamoto inayotutesa muda wote kuhusu maswala ya kihabari na kitengo cha Habari na Mawasiliano cha Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma
Kutokana na hali hiyo tuliamua mimi na kamati yangu  kuwaita maafsa wa habari na mawasiliano wa taasisi zote kubwa za kiserikali na za binafsi ambapo tuliomba ukumbi na tukapewa kwa maandishi katika ofisi za mkuu wa mkoa cha kushangaza ni kuwa hakukuwa na mwakakilishi yoyote toka ofisi hiyo, hivyo tunakuomba mkuu wa wilaya utufikishie ujumbe wetu kwa mkuu huyo ili azifanyie kazi”, alisema
Aidha alisema kuhusu ubaguzi wa vyombo vya habari kwa kutaka kufanya kazi na vyombo ambavyo yeye anaita vikubwa vya Luninga na baadhi ya Magazeti bila kutaka kufanya kazi na redio za kijamii zilizopo mjini Dodoma wakati hivyo ndivyo vinasikika vijijini na maeneo yasiyo na umeme bila tatizo
Kwa Upande wake Mkuu wa Wilaya Chirstina Mndeme aliwataka waandishi hao kutokatishwa tama na baadhi ya watu hasa linapokuja swala la kutaka kuwahabarisha watanzania huku akiwataka wanadodoma kuwa wazalendo kwa kuanza na kupenda vya kwao ikiwemo kuzigeuza changamoto kuwa fursa 

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG