Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara
inatarajiwa kuendelea leo Februari 2, mwaka huu ambako Mwadui itaialika
Ruvu Shooting kwenye Uwanja wa Mwadui, Shinyanga.
Mchezo huo pekee Na. 201 utaanza
saa 10,00 jioni na Ijumaa Januari 3, Young Africans ya Dar es Salaam,
itaikaribisha Stand United ya Shinyanga kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es
Salaam wakati Jumamosi Februari 4, mwaka huu kutakuwa na mechi mbili.
Mechi za Jumamosi zinatarajiwa
kuwa ni kati ya Mbeya City na JKT Ruvu kwenye Uwanja wa Sokoine jijini
Mbeya wakati Majimaji itakuwa mwenyeji wa Simba katika mchezo
utakaofanyika Uwanja wa Majimaji mjini Songea.
Jumapili kutakuwa na mchezo kati
ya Azam FC na Ndanda FC kwenye Uwanja wa Chamazi ulioko Mbande – mchezo
unaotarajiwa kuanza saa 1.00 usiku.
Jumatatu kutakuwa na mchezo mmoja tu ambako Toto Africans ya Mwanza itaikaribisha Ruvu Shooting ya Pwani kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Wikiendi ya Februari 10, 11 na 12 hakutakuwa na mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom badala yake wawakilishi wa Tanzania katika mchuano ya kimataifa Young Africans (Michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika – CL) na Azam (Kombe la Shirikisho – CC) watakuwa na mechi na mechi za kimataifa.
Jumatatu kutakuwa na mchezo mmoja tu ambako Toto Africans ya Mwanza itaikaribisha Ruvu Shooting ya Pwani kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Wikiendi ya Februari 10, 11 na 12 hakutakuwa na mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom badala yake wawakilishi wa Tanzania katika mchuano ya kimataifa Young Africans (Michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika – CL) na Azam (Kombe la Shirikisho – CC) watakuwa na mechi na mechi za kimataifa.
Tags
MICHEZO KITAIFA