BANDA MEDIA BLOG

VIJANA WATAKA VITA YA DAWA ZA KULEVYA IWE YA WATANZANIA WOTE.


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam


Vijana kutoka Asasi mbalimbali za kijamii nchini wameshauri Wakuu wa Mikoa yote hapa nchini kutekeleza agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli la kupambana na watumiaji na wasambazaji wa dawa za kulevya.

Vijana hao wametoa kauli hiyo leo jijini Dar es salaam wakati wa mkutano na waandishi wa habari juu ya kuunga mkono juhudi zinafanywa na uongozi wa Serikali ya Awamu ya Tano.
Wamesema mapambano dhidi ya dawa za kulevya siyo ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam pekee Paul Makonda, yapaswa yafanywe na viongozi wote wakiwemo Mawaziri, Wabunge, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na wananchi wenye kupenda maendeleo mema ya nchi hiyo.
Wametoa wito kwa wananchi kusaidia katika utoaji wa taarifa za watu wanaojihusisha na biashara hiyo haramu ya dawa za kulevya katika Ofisi zao za Mitaa.
Wameongeza kuwa Tanzania ya Viwanda haiwezi kufanikiwa ikiwa nguvu kazi inaharibika kutokana na matumizi ya dawa  za kulevya na kuwageuza vijana ambao ndio tegemeo kuwa tegemezi.
Aidha vijana hao wameonya baadhi ya Viongozi na Wanasiasa kuacha tabia za kuwakatisha tamaa viongozi waliojitoa kupambana na biashara hiyo haramu kama vile Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda.
Wasema kuwa kufanya hivyo kunawatia mashaka na kuwahisi kuwa wao na ni wahusika katika biashara hiyo haramu ambayo inaliteketeza Taifa.
Vijana hao wametoa siku tatu kwa wafanyabiashara wakubwa kujisalimisha wenyewe la sivyo watawataja.
Vijana waliounga mkono juhudi za Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam wanatok

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG