BOT YAONYA WANAOTUMIA PESA KUTENGENEZA MASHADA/MAUA
BENKI Kuu ya Tanzania (BoT) imeonya matumizi mabaya ya pesa ikiwemo wale wanaotumia pesa hizo kutengeneza mashada na maua kwa ajili ya kuwatunuku wapendwa wao kwenye Sherehe Mbalimbali
“Tuligundua maeneo mengi tu ya nchi utakuta noti zinatengenezewa mashada, zinatengenezewa maua, watu wengine wanatupa chini pesa au labda mtu anatoa burudani ile noti inachukuliwa inaenda kubandikwa sehemu yenye jasho, kichwani, kwenye paji la uso. Mnapofanya hivyo mnakiuka sheria,” amesema Meneja Msaidizi Kitengo cha Mawasiliano BoT, Noves Moses
