Sehemu ya Washiriki wa Kongamano hilo lililozihusisha Asasi zisizo za kiserikali
Sehemu ya Washiriki wa Kongamano hilo lililozihusisha Asasi zisizo za kiserikali
Sehemu ya Washiriki wa Kongamano hilo lililozihusisha Asasi zisizo za kiserikali
Baadhi ya washiriki wa Kongamano hilo wakijitambulisha
Baadhi ya washiriki wa Kongamano hilo wakijitambulisha
Baadhi ya washiriki wa Kongamano hilo wakijitambulisha
Washiriki wakinyoosha viungo wakati wa Kongamano hilo
Wakili Mary Munis akizungumza jambo kwenye Kongamano hilo
Ofisa Programu kutoka Jukwaa la Katiba Tanzania, (JUKATA) Thobias akizungumza na vyombo vya habari
....................................................................
NA JOHN BANDA, DODOMA
MAKAMU wa rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika
(TLS) Wakili Deus Nyabiri amezitaka asasi za kiraia kuwa na uelewa wa kazi
wanazozifanya kwenye Jamii.
Pia imeelezwa kuwa matukio ya ‘unyanyasaji’ dhidi ya
watendaji wa mashirika ya kiraia yamepungua kwa kiasi kikubwa kati ya 2021 na
2023.
Nyabiri Amesema hayo December 12,2023 wakati
akifungua semina ya kuzijengea uwezo asasi za kiraia kuhusiana na masuala ya
utawala bora iliyoandaliwa na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS).
Amesema kuwa kuna umuhimu mkubwa kwa asasi za kiraia
kuelewa wanachokifanya ili kuelimisha Jamii kwani wao ni kiungo muhimu kati ya
wananchi na Serikali.
“ Sasa tunakaribia kwenda kwenye uchaguzi je asasi
zinajua mambo yanayohusiana na uchaguzi? zinajua sheria, kanuni za uchaguzi,
mabadiliko yanayotokea, ,?, ” amesema na kuhoji
Wakali huyo Amesema, kuna haja kwa kila asasi kujua
wajibu wake, ili kuweza kutekeleza mipango na miradi yao kwa ufanisi, kwa
maslahi yao, serikali na wananchi.
Amesema ni vyema kwa kila asasi za kiraia, zikawa na
ubobezi kwa kile wanachokitekeleza, ili kuwe na ufanisi wa kuleta mabadiliko
kwenye jamii na taifa kwa ujumla..
Kwa upande wake, Mshauri Mwelekezi wa masuala ya
maendeleo, sekta ya Asasi za Kiraia (AZAKi), Sia Ngowo Amesema utafiti wa
msingi juu ya mazingira ya Sera ya Kisheria kwa Ushirikishwaji wa AZAKi, katika
Utawala wa Kidemokrasia ulifanyika Tanzania Bara na Zanzibar (Mei na Juni 2023).
Ngowo Amesema kuwa lengo la utafiti huo lilikuwa ni
kukusanya taarifa za msingi kuhusu sheria, sera, na fursa za kiutendaji na
changamoto za ushiriki wa AZAKi katika utawala wa kidemokrasia.
Amesema jumla ya watu 311 walishiriki huku asilimia
44.6wakiwa wanawake, taasisi zaidi ya 60 pia Wadau wengine walijumuisha maofisa
wa umma na wawakilishi kutoka sekta binafsi (vyombo vya habari na mashirika ya
kisheria).
Amesema katika utafiti huo, walibaini kuwa AZAKi
zinakabiliwa na changamoto katika kutekeleza utetezi unaozingatia ushahidi.
Pia upatikanaji wa nyenzo muhimu kwenye nafasi ya
kiraia ni mdogo kwa asilimia 46, asilimia chini ya tano ya AZAKi zinafanya
tafiti kuhusu hali ya maeneo ya kiraia.
“Ripoti za kina za hali kuhusu wanawake, vijana, na
watu wenye ulemavu hazipo kabisa,” amesema.
Aidha amesema asilimia 70 ya AZAKi zinakabiliwa na
matatizo ya kifedha, jambo linalozuia uchangamfu na ushiriki wao.
“Ufadhili unazidi kuwa changamoto, huku asilimia 68
ya AZAKi zikipokea ruzuku kutoka kwa mashirika matatu tu ya ndani, kama vile
Foundation For Civil Society na LSF,” amesema.
Abainisha kuwa kuna haja ya kuwepo kwa majukwaa rasmi
ya ushirikiano kati ya AZAKi na serikali, ikiwa ni pamoja na yale ya kisheria,
ambayo yanatoa njia za ushirikiano na mazungumzo.
Akizungumzia hali ya uzingatiaji wa AZAKi, Sia
Amesema kuwa asilimia 32, ya AZAKi zilionyesha uelewa wa hali ya juu. Asilimia
56 wana kiwango cha wastani cha ufahamu. Pia uelewa mdogo unaohusishwa zaidi na
AZAKi za vijijini - kutokana na upatikanaji mdogo wa habari.
“Pia asilimia 63 ya AZAKi, zimeridhika na mahitaji ya
sasa, Kuongezeka kwa ujuzi na usimamizi wa taratibu za kufuata.
Pia asilimia 59, ya AZAKi zilitambua taratibu changamano
za kufuata kama suala la msingi, linaloathiri uzingatiaji.Asilimia 35 ya AZAKi
zilitambua masuala yanayohusiana na gharama, kama vile ada nyingi, kodi na
tozo, kama suala jingine kuu linaloathiri uzingatiaji.
Amesema asilimia 8. Tu ya AZAKi zinazohusika katika
vikao vya kujenga uwezo ili kuongeza uwezo na uelewa.
Pia AZAKI, za vijijini zinakabiliwa na changamoto za
kupata barua pepe kwa wakati.
“Katika kipengele cha Uthabiti wa Mifumo ya Kisheria:
Hakuna mabadiliko makubwa ambayo yamefanywa kwenye mifumo ya kisheria,
inayoongoza jumuiya za kiraia Tanzania Bara na Zanzibar tangu mwaka 2021,”
amesema
Pia amesema kuwa kuna upole unaoonekana katika
kutekeleza sheria na kanuni na vifungu 'kandamizi'.
“Matukio ya ‘unyanyasaji’ dhidi ya watendaji wa
mashirika ya kiraia yamepungua kwa kiasi kikubwa kati ya 2021 na 2023.
Ameweka wazi kuwa mikataba muhimu, kama vile CAT,
Itifaki ya Afrika ya Uchaguzi na Demokrasia, na Itifaki ya Walemavu,
haijaidhinishwa na kupitishwa nchini hadi 2023.
“Asilimia 44 ya AZAKi mara nyingi hushirikiana na
serikali katika shughuli zao., pia asilimia 42 ya AZAKi wakati mwingine
hushirikiana na serikali. asilimia 8 ya AZAKi hushiriki mara chache, wakati
asilimia 4 hawajihusishi na serikali,” amesema
Pia ameongeza takribani asilimia tano tu ya
AZAKi zilizo na hati iliyoandikwa ya mkakati wa ushiriki wa washikadau/ubia. na
asilimia 46 ya AZAKi mara nyingi hushiriki katika mikutano ya kawaida na
serikali, asilimia 31 mara nyingi hushiriki katika mashauriano ya kiufundi,
asilimia 30 mara nyingi hujihusisha na majukumu ya
uangalizi wa kawaida, kama vile ufuatiliaji na serikali.
Asilimia 19 mara nyingi hushirikiana na serikali
katika kuunda uingiliaji wa pamoja.
Naye Ofisa Programu kutoka Jukwaa la Katiba Tanzania,
(JUKATA) Thobias amesema kuwa wapo tayari kutoa mapendekezo juu ya mabadiliko
ya sheria ya Asasi za kiraia ambayo inataka kila baada ya miaka 10, kusajiliwa
upya kwani hilo litaleta migongano kati yao na wafadhili.
Pia aliishukuru serikali ya awamu ya sita kwa
kuwaunganisha na serikali.
mwisho