WANAWACHAMA WA DOWOSA WATAKIWA KUWA WASTAARABU NA WAVUMILIVU ILI MALENGO KUSUDIWA YAWEZE KUFIKIWA
Wajumbe wa Bodi Hiyo ni Mwenyekiti Kituina Kippa, Makamo Mwenyekiti Justina Mashiba pamoja na Tumaini Sanga, Penina Mnyaki na Elizabert Kasimika ambao ni wajumbe, huku kamati ya Usimamizi Anjelina Sanga, Grace Chigongolo na Mary Mabaya.
.JPG)
Kura zikipigwa
Mkutano ukiendelea
Sehemu ya Wajumbe wa mkutano huo
.............................................. NA MWANDISHI WETU,
BANDA MEDIA
ONE.COM,DODOMA
MWENYEKITI mteule wa
chama cha Ushirika na Mikopo cha DODOMA Woman Saccos, (DOWOSA) Kituwina Kipa
amesema ili chama hicho kiweze kutimiza malengo kusudiwa inabidi wanachama wake
wawe wastaarabu na wenye kupenda ushirikiano.
“ili Saccos hii iweze
kutimiza Malengo yaliyokusudiwa ya kumkomboa mwanamke kiuchumi inabidi kuacha uswahili, kuwa wavumilivu, wapende
kushirikiana na kuzingatia ustaarabu”, amesema
Kipa ameyasema hayo
wakati alipokuwa akifunga mutano wa Uchaguzi wa viongozi wa DOWOSA uliofanyika
Desenba 21,2023 jijini Dodoma ambapo wanachama waliwachagua wajumbe wa Bodi na
kamati ya Usimamizi.
amesema hakuna mtu
anayetamani kufanya vibaya, Tusilete Uswahili bali Uswahili tuuache huko mitaani
maana sisi sote ni wastaarabu na tunataka maendeleo kupitia saccos yetu’’,
Aidha amesema baada ya
Uchaguzi huo kukamilika sasa kazi za Saccos Zinaanza Rasmi na hivyo kuwataka
wanachama wote kumalizia kununua Hisa ili waweze Kukopesheka
“kila mtu amepita pale
nje ameona jina lake na kiasi cha hisa alizonunua, niombe kama tulivyokubaliana
kila mtu anunue hisa 10 ambazo ni tsh. 100,000 Laki moja na pia aweke Akiba
yake ili iwe rahisi kukopeshwa.
Awali Mgeni Mualikwa
Asha Towfik ambaye ni Mbunge wa Viti maalumu Mkoa wa Dodoma, amesema Saccos
Hiyo itawakomboa wanawake kuondokana na mikopo ya kausha Damu ambayo imepelekea machafuko na kuvunjika kwa ndoa za
baadhi ya wanawake waliojihusisha na Mikopo hiyo, kutokana na liba kubwa ambapo
DOWASA Itatoza asilimia moja peke .
Waliochaguliwa kuwa
wajumbe wa Bodi Hiyo ni Mwenyekiti Kituina Kipa, Makamo Mwenyekiti Justina
Mashiba pamoja na Tumaini Sanga, Penina Mnyaki na Elizabert Kasimika ambao ni
wajumbe, huku kamati ya Usimamizi Anjelina Sanga, Grace Chigongolo na Mary
Mabaya.