WIKI YA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAADILI NA HAKI ZA BINADAMU YAENDELEA JIJINI DODOMA, HUKU WANANCHI WAKIMIMINIKA KUTAFUTA MSAADA WA KUPATA HAKI ZAO ZA ARIDH
...............................................................
NA JOHN BANDA, DODOMA
IMEBAINIKA kuwa migogoro ya Aridh jijini Dodoma
Bado ni Donda Ndugu Kutokana na wananchi walio wengi kuendelea kumiminika katika
Mabanda ya maonyesho yanaotoa Elimu mbalimbali ikiwemo haki za Binadamu kupitia
umiliki Aridh.
Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya
Raisi, Menejimenti ya Utumishi wa UMMA na Utawala Bora, Anayeshuhulikia Ukaguzi
na Maadili katika Idara ya Usimamizi wa Maadili, Ally Abdu Ngowo alipoongea na
waandishi wa habari, Jijini, Dodoma wakati akiambatana na baadhi ya viongozi wa
taasisi simamizi kukagua namna taasisi zilizojitokeza kutoa huduma katika wiki
ya maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu yanayoendelea Jijini humo
Ngowo Amesema Uzoefu walioupata baada ya Kumaliza
kutembelea Mabanda hayo wamebaini kuwa, Migogoro ya Aridh Bado ni changamoto
kubwa jijini humo lakini serikali imeboresha utoaji huduma Kwa kuanzisha
Kliniki ya Aridh Kupitia Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma
Aidha amesema kuwa Kwa upande Mmoja wananchi wamekuwa
wakichangia kusababisha migogoro hiyo kutokana na kuuza mashamba au viwanja
zaidi ya mara moja
" Nitoe wito Kwa wananchi kuacha kuuza Aridh zao
Kwa mtu zaidi ya mmoja, pia hata upande wa wataalamu wetu wa Aridh waache
kufanya zile (Double Allocation) ili kuindoa migogoro hiyo",
amesema
Ameongeza kuwa tume hiyo ina Imani ya kuondoa Mianya
ya Rushwa, kutokana na Mpango wa uanzishwaji wa Mfumo wa TEHAMA ambao utanyesha
wamiliki wa kila kiwania na mashamba.