PICHA zinaonyesha Tayari Wiki ya Sheria imeanza wananchi na viongoizi mbalimbali wanatembelea mabanda na kupata Elimu Stahiki.
............................................................
NA JOHN
BANDA, DODOMA
SPIKA wa Bunge
la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Tulia Akson Kesho Januiari 27,2024 anatarajiwa
kuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa wiki ya sheria katika viwanja vya nyerere
square jijini Dodoma
Ambapo kwa
mujibu wa ratiba iliyotolewa na Mtendaji
Mkuu wa Mahakama inaonesha kuwa maadhimisho ya wiki ya sheria inaanza januari
24 hadi 30 mwaka huu ikijumuisha wadau wa haki jinai na taasisi nyingine za serikali
na sekta binafsi
Maadhimisho
hayo yanayojumuisha taasisi 45, wakiwemo wadau wa haki jinai na taasisi
nyingine za kiserikali pamoja na sekta binafsi,kuelekea wiki na siku ya sheria
ambayo huadhimishwa februari 1 kila mwaka Dkt. Tulia atashiriki Matembezi ya km. 10
Pamoja na
mambo mengine katika uzinduzi huu Dkt.Tulia atazindua Mfumo wa transcription
and Translation system(TTS)na baadae kuwahutubia wadau wa sheria haki
jinai,watendaji wa Mahakama na wananchi wa ujumla