BANDA MEDIA BLOG

No title

 

JESHI LA POLISI LAWATAKA WAMILIKI WA SHULE KUPELEKA MAGARI YA KUSAFIRISHIA WANAFUNZI YAKAKAGULIWE.



            ....................................................................

               Na Mwandishi Wetu DODOMA.

                 BANDA MEDIA ONE.COM

ILI kuhakikisha Usalama wa wanafunzi kwenye vyombo vya Usafiri Jeshi la polisi kikosi cha usalama barabarani Jijini Dodoma limekuja na mkakati maalum wa kuwaandikia barua za wito wamiliki wote wa Shule Binafsi na zile zinazotumia magari kwa ajili ya kubebea wanafunzi kuyapeleka magari yote yakakaguliwe

Hayo yamebainishwa hii  leo Janualy 4,2024  jijini humo na Koplo Ester Makali kutoka Ofisi ya Mkuu wa kitengo cha Usalama Barabarani Dawati la Elimu kwa UMMA Mkoa wa Dodoma, wakati akiongea na waandishi wa habari, ambapo amesema Jeshi hilo limejipanga kuhakikisha Magari yote yanayotoa huduma hiyo yanakuwa na Ubora Unaotakiwa kuelekea mwaka mpya wa masomo.

Koplo Makali amesema tayari Barua hizo zimeanza kusambazwa kwa Wamiliki wa Shule hizo  na kwamba Magari yote ambayo hayatakaguliwa hayataruhusiwa Kutoa huduma hiyo Muhimu kwa Watoto.

“Tumewambia wamiliki wote wa shule zinazotumia usafiri wa mabasi kwa wanafunzi, wahakikishe wanayeleta Magari yote tuyakague kabla ya kukunguliwa kwa Shule hapo Januali 8, na kila Mmiliki anatakiwa kutii Sherea Bila Shuruti, na kwamba baada ya hapo tutaendelea kuyakagua kila mara wakati yakiendelea kubeba watoto,

Tumeamua kufanya hivyo kwa lengo la Kuondokana na ajali zisi za lazima lakini pia, wakati mwingine magari hayo yanapohalibika hovyo Barabarani inawafanya watoto kukosa haki yao ya msingi kujaliwa na kupata Elimu sawa na ratiba ya Shule”, amesema

 Ameongeza kuwa Dereva yoyote atakayekamatwa akiwa amepakia watoto zaidi kwenye Siti moja atachukuliwa hatua za kisheria ikiwemo kutozwa faini ya makosa ya Barabarani.

Aidha amsema kuwa wamekuwa wakitoa elimu kwa Madereva wa Magari hayo kutokubali kupokea magari mabovu kutoka kwa wamiliki wa shule lakini wamekuwa wakishindwa kufanya hivyo kwa kigezo cha ugumu wa Maisha kwani  hali hiyo imekuwa ikiwasababishia wao kupata Usumbufu wa kuhalibikiwa barabarani au kupa ajari.

Baadhi ya Wazazi na Walezi akiwemo Agatha Mataze Mkazi wa Mkoze Jijini Dodoma wamesema jambo liningine lakuangaliwa ni namna ya kudhibiti mwendo kasi wa baadhi ya madereva ambao wakati mwingine wamekuwa wakiendesha magari hayo kama wapo kwenye mashino..

Kutona na Shule kufungwa katika kipindi hiki Juhudi za kuwatafuta na kuwapata wamiliki wa shule hizo  ili watueleze jinsi walivyojipanga zimegonga mwamba, japo juhudi kuwatafuta  zinaendelea… 

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG