SHULE 68 ZA SEKONDARI ZISIZO ZA SERIKALI ZILIZOIDHINISHWA KUTEKELEZA MTAALA WA AMALI KUANZIA JANUARI 2024
.......................................................
NA MWANDISHI WETU
BANDA MEDIA ONE.COM
Wizara ya
Elimu, Sayansi na Teknolojia (WyEST) kupitia NECTVET imezitaja Shule za
Sekondari zisizo za Serikali zilizoidhinishwa kutekeleza Mtaala wa Amali,
kuanzia Januari hii, 2024.
Taarifa iliyosainiwa na Kamishna wa Elimu Dk. Lyabwene Mtahabwa imesema shule
hizo ni ambazo WyEST kupitia NETVET imefanya tathmini katika shule za sekondari
zilizopendekezwa kutekeleza mtaala huo ili kujiridhisha na maandalizi
yaliyofanyika kwa ajili ya kuanza utekelezaji Januari 2024.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Wamiliki wa shule husika wanatakiwa kuwaelekeza
wakuu wa shule kwa kushirikiana na Wazazi/Walezi katia kufanya maamuzi ya
uchaguzi wa mikondo ambayo wanafuzi wa kidato cha kwanza mwaka 2024 watasoma.
