BANDA MEDIA BLOG

SPIKA DKT. TULIA AWASHAURI WADAU WA HAKI JINAI KUUNGANA KATIKA UTOAJI HAKI



SPIAKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania DKT. Tulia Akson amewashauri Wadau wa Haki jinai kuhakikisha wanaenda na kasi waliyo nayo mahakama ili kurahisisha utoaji wa Haki kwa wananchi wanaostahili kuipata

Dkt, Tulia ametoa ushauri huo wakati akizindua maadhimisho ya Wiki ya Sheria leo Januari 27, 2024 katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma, uzinduzi huo ukitanguliwa na matembezi ya km 10 yaliyowahusisha wadau mbalimbali wa Haki jinai, Taasisi mbalimbali za Serikali, Sekta Binafsi wakiwemo wananchi wa jiji la Dodoma.

Amesema Mahakama ya Tanzania imeimarisha Mfumo wa TEHAMA kwa kuanzisha Mfumo wa Akili Bandia kwa Lengo kuharakisha utoaji wa haki, hivyo kila mdau wa haki jinia wakiwemo Polisi, Magereza, Takukuru na vyombo vingine vya utoaji haki wahakikishe wanaungana na Mahakama.

“wadau wengine wa haki jinai tuhakikishe tunaungana na wenzetu ili tukaharakishe kutoa haki kwa wananchi na yoyote ambaye atasuasua atakuwa akiichelewesha mahakama kutoa haki kwa wakati kwa yule anayestahili”Amesema

Aidha Spika amempongeza Mtendaji mkuu wa Mahakama kwa kuja na mfumo wa Akili Bandia kwa ajili ya kurahisisha Utoaji wa Haki kwa wakati  na kuitaka mahakama kuwa na utayari wa kupokea kesi za watu ambao watalalamika kubambikiwa ushahidi na Mfumo huo.

Awali  Mtendaji mkuu wa Mahakama Elsante Ole Gabriel amesema mfumo huo wa unukuzi na tafsiri unatafsiri lugha mbili zinazotumiwa na watanzania ikiwemo kiswahilki na kiingereza kwa kufuata lafudhi ya makabila ya watanzania ambao kwa sasa imeshafungwa katika vituo 11 hapa nchini.





 

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG