Mpira wa Pete nao Ukapigwa
Wabunge mashabiki wa Yanga na Simba wakavishwa Medari za Ushiriki
Dkt, Tulia amebainisha hilo
wakati alipokuwa akizungumza na wabunge, watumishi wa Bunge pamoja na watumishi
wa taasisi nyingine za serikali na zisizo za kiserikali kwenye uwanja wa
jamhuri Jijini Dodoma mara baada ya Wabunge mashabiki na wanachama wa Timu za
Simba na Yanga Kumaliza kupapatuana kwenye Michezo mbalimbali.
Amesema mwezi wa nne Mwaka huu
kutakuwa na Bunge Marathoni itakayowahusisha wadau pamoja na wananchi wa majimbo
mbalimbali kujiunga na kushiriki ili kufanikisha ujenzi wa Shule ya Sekondari
ya Bunge ya Wavulana itatangazwa baadae kuwa itajengwa wapi, mbayo itakuwa kama
ile ya wasichana iliyojengwa Kikombo jijini Dodoma kutokana na fedha walizozipata
kutokana na Bunge marthoni ya miaka ya hivi karibuni.
Amesema kila mshiriki
atatakiwa kujiunga kwa kuchangia 40,000
“niombe watu wengi wajitokeze
kutoka kwenye majimbo ambako wanatoka wabunge, ambapo ukiwa hapa utakimbia na
Mbunge wako pamoja na wabunge wengine na hata mimi watu kutoka kwenye jimbo
langu wakija nitakimbia nao”, amesema
Kwenye Bonanza hilo
lililojumuisha michezo mbali,mbali wabunge na mashabiki wa Yanga wameibuka kuwa
washindi wa jumla kutokana na kushinda michezo mbalimbali ukiwemo mpira wa
miguu ambayo waliwabugiza wenzao wa simba jumla ya Goli 5.kwa 4 kupitia
changamoto ya mikwaju ya penati baada ya
dakika za kawaida kutoshana nguvu kwa kutoka sare ya 1.1
Bunge Spoti Bonanza
imedhaminiwa na AZANIA BENK waliyowezesha maandalizi kabambe ikiwemo kuufunika uwanja wa
jamhuri jijini Dodoma kwa Mango huku Shirika la Ndege La QATAR AIRWAYS likitoa
zawadi kwa Mbunge mmoja mshindi Tiketi ya Busness Class kwenda na kurudi nchi
yoyote Dunia atakayochagua