BANDA MEDIA BLOG

Tanzania yaagiza sukari nje, kudhibiti uhaba wa bidhaa nchini

 

 

Waziri wa Kilimo nchini Tanzania Hussein Bashe

Waziri wa Kilimo nchini Tanzania amesema serikali imechukua hatua kadhaa kuhakikisha uhaba wa tatizo la uhaba wa sukari nchini linaondoka. Waziri Bashe amesema, miongoni mwa hatua hizo, ni pamoja na kutoa vibali vya kuruhusu uingizaji wa sukari takriban tani laki moja kutoka nje.

Kauli hii ya serikali, inakuja baada ya bidhaa hiyo muhimu kupanda bei kutoka shilingi elfu mbili hadi elfu nne na katika baadhi ya maeneo kuadimika kabisa. Hali ambayo imeibuwa wasiwasi kwa wananchi kutokana na umuhimu wa bidhaa hiyo ambayo mahitaji yake kwa siku ni takriban lakini 1500 kwa siku.

"Hatua ya kwanza tuliyochukua kama serikali, ni kuruhusu uagizaji wa sukari wastani wa tani laki moja ambao tumewapa viwanda ili waweze kuingiza hiyo sukari, maamuzi ya kuwapa viwanda sio ya bahati mbaya, kama mnavyofahamu, ni lazima tulinde viwanda vyetu vya ndani, na hatulindi kwa gharama ya mlaji, bei ya sukari kabla ya tatizo hili, viwandani ilikuwa bei 2240 mpaka 2270 na bei ya reja reja ilikuwa inatembea kati ya 2700 mpaka 3000, leo imepanda baadhi ya maeneo mpaka kufika 4000. serikali tumewaagiza viwanda kusimamia kuhakikisha kwamba wanasimamia usambazaji wao kama kawaida bila kumuumiza mlaji. Lakini hatua ya pili tuliyochukua kama serikali, tumetoa idhini ya uagizaji wa sukari zaidi ya tani laki moja, tunaamini hii ikiingia katika mfumo wetu wa ugavi, hali ya usambazaji wa sukari itakuwa katika hali nzuri," amesema Bashe.

Tanzania ina jumla ya viwanda saba vya sukari, ambapo kwa mujibu wa serikali, kutokana na mvua kubwa zinazoendelea katika maeneo mbalimbali nchini humo, uzalishaji umepungua kwa takriban tani elfu moja kwa siku.

Waziri huo amefafanua kuwa, katika kipindi cha mvua, mbali na uvunaji na uchakataji wa sukari unavyokuwa mgumu, lakini kiwango pia cha sukari katika miwa kinapungua kwa zaidi ya asilimia 25.

 


Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG