Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa CCM Tanzania (UWT), Mary
Chatanda akihutubia wakati wa kufunga semina Kikundi cha Wabunge
Vinara Wanawake katika Siasa iliyofanyika jijini Dodoma ambapo walijadili
namna ya kwenda kuongeza ushiriki na uwakilishi wa wanawake katika
uongozi na siasa kupitia miswada mitatu inayopelekwa bungeni. Mwenyekiti wa
kikundi hicho ni Mbunge wa Viti Maalumu, Neema Lugangira.
......................................................
WABUNGE wanawake wametakiwa kumtua mzigo begani Rais Samia Suluhu Hassani kuhusu uwepo wa sheria sahihi inayojali usawa wa kijinsia katika uongozi mbalimbali.
Msisitizo huo umetolewa na Wajumbe wa Kamati Kuu ya Chama Chama Mapinduzi CCM, Halima Mamuya na Mary Chatanda wakati wa semina ya Kikundi cha Wabunge Vinara Wanawake katika Siasa iliyofanyika jijini Dodoma ambapo walijadili namna ya kwenda kuongeza ushiriki na uwakilishi wa wanawake katika uongozi na siasa kupitia miswada mitatu inayopelekwa bungeni.
Naye Mamuya aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa UWT, amesema kuwa wabunge wanawake na viongozi wengine kupambania usawa wa kijinsia siyo ombi bali ni lazima tuhakikishe tunamtua mzigo begani Rais Samia.
