BANDA MEDIA BLOG

WAKAZI DAR WALIA MAAFA YA MAFURIKO


Nyumba kadhaa zimefunikwa na maji. Picha/TRT Afrika. 
Mvua iliyonyesha kwa zaidi ya saa kumi, imeleta uharibifu wa mali, miundombinu pamoja na baadhi kupoteza maisha. Picha/TRT Afrika

 Watu kadhaa wanaripotiwa kupoteza maisha  jijini Dar es Salaam, nchini Tanzania baada ya mvua kubwa kunyesha nchini humo kwa zaidi ya saa kumi. Hayo ni kwa mujibu wa mwandishi Wetu

Maeneo yanayoripotiwa kuathirika zaidi ni katika viunga vya mji huo kama vile Mbezi, Tegeta, ambapo nyumba kadhaa zimefunikwa na maji, huku baadhi ya vitu kama magari, matawi ya miti pamoja ambapo mali kadhaa zikisombwa na mafuriko.

Mvua hizo pia, zinaripotiwa kuharibu miundombinu muhimu ya barabara ikiwemo kuvunja Daraja la Mtongani ambalo ndilo kiunganishi kikubwa cha mji wa Dar es Salaam mji wa kihistoria wa Bagamoyo uliopo Mkoa wa Pwani.

Baadhi ya wakazi wa mji huo wa kibiashara, ambao unaongoza kuwa na idadi kubwa ya wakazi zaidi ya milioni tano, wanakiri kwamba shughuli zao za kila siku zimekwama kutokana na uharibifu wa mali uliosababishwa na mvua hizo.

Maafa hayo yanatokea ikiwa imepita mwezi mmoja na wiki kadhaa tangu kutokea maporomoko ya udongo huko katika Wilaya ya Hanang, Kaskazini mwa Tanzania ambayo yalisababisha vifo vya zaidi ya watu 80, huku mamia wakiachwa bila makazi.

Awali, Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini humo ilitoa tahadhari ya kuwepo kwa mvua kubwa, maarufu El Nino na kutaka watu hasa wale wanaoishi karibu na mabonde kuchukua tahadhari. Wataalamu wametabiri eneo la Afrika Mashariki kukumbwa na mvua hizi, ambazo kwa kawaida huwa ni nyingi kupitiliza na huleta madhara kwa wananchi kutokana na mafuriko, pamoja na maporomoko.

 


Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG