Prof. Fadhil Mgumia akimkabidhi zawadi ya ushindi wa kusoma Qur'an kwa ufasaha Mwanafunzi kutoka Chuo cha Saint John Hassan Suleimani aliyeibuka Mshindi na kuzawadiwa cheti na Fedha Taslimu.
………………………………………………………
NA JOHN BANDA, DODOMA
MASHINDANO ya Qur’ an kwa wanafunzi wa Vyuo vikuu na
vya kati Mkoani Dodoma yamefanyika Aprili 6,2024 ikiwa zimesalia siku chache
kukamilika kwa Mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani huku msisitizo ukiwa ni kwa
waumini wa Dini ya Kiislamu kuendea kuyaishi mafunzo waliyoyapata.
Akizungumza baada ya mashindano hayo Mlezi wa Wanafunzi
wa Kiislamu wa Chuo cha Mipango, Prof. Fadhil Mgumia amesema mwezi wa Ramadhin Umejaa Kheri nyingi, Rehema
Nyingi ni mwezi Mtukufu na ni mwezi wa Mfunzo ambapo Waumini hufanya Ibada
Nyingi wakitoa na Sadaka.
“mwezi huu ni kama chuo tunafundishwa namna ya kuishi
kama waislamu, basi hata mwezi unapoisha tuendelee kuwa waislamu tunaosali,
kutoa sadaka, kusoma QUR’AN na kuendelea kushindana katika kuisoma,
Kama mwezi Mtukufu wa Ramadhan ni Chuo nategemea
mwezi utakapoisha tutaendelea na yale tuliyofundishwa ndani ya mwezi huu”,
amesema
Awali Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano hayo Fahmi Ali Hassan amesema jumla ya wanafunzi 31 kutoka vyuo vya UDOM, Serikali za Mitaa Hombolo, St. John na Mipango yenyewe ndiyo walioshiriki huku mwanafunzi kutoka Chuo cha Saint John Hassan Suleimani akiibuka Mshindi na kuzawadiwa Fedha Taslimu.
Mmoja wa waalikwa kwenye mashindano hayo mkurugenzi wa Wema Takaful Agency Ltd, wakala wa kampuni inayotoa huduma za kibima kwa kuzingatia Shariah ya Kiislam ndugu Ally Ally amewataka Waislamu na Watanzania kwa ujumla kujiunga na Bima hiyo
Amesema Bima hiyo inakidhi viwango kwa kuzingatia makatazo
yote ya kisheria kwani haina Riba wala kupoteza kama kucheza kamali isiyo na
udanganyifu.
ukikata Bima hii unashiriki katika mfumo wa uchumi unaoafikina
na Sheria za nchi, mteja hawezi kupoteza kama aliyecheza kamali, inatoa gawio
kila mwaka kwa mteja ambaye hajadai, inakuza maadili na uwajibikaji kwa jamii lakini
pia anashiriki katika uwajibikaji wa Pamoja na kupata gawio la faida”, amesema