BANDA MEDIA BLOG

VIONGOZI WA USHIKIKA WA MAMA WA KIKRISTO WAHAMASISHWA KUGOMBEA SEREKALI ZA MITAA

 

Mratibu wa Dawati la Maendeleo ya Wanawake, Jinsia na Watoto CCT,  Shemasi Ester Mahagachi akielekeza jambo wakati alipokuwa akifunga mafunzo ya Uongozi, Uundwaji wa Vikundi na Usimamizi wake yaliyofanyika jijini Dodoma

Rey Conon Dkt. Margareth Ndonde ambaye pia ni Katibu wa Wanawake wa Kanisa la Anglikana Tanzania akiimba pamoja na washiriki wa mafunzo hayo wimbo wa Tanzania Nakupenda uliomo katika Albamu yake yenye nyombo 8 ikienda kwa jina la Mungu wetu ni wa Ajabu

..........................

NA JOHN BANDA, DODOMA

MRATIBU wa Dawati la Maendeleo ya Wanawake, Jinsia na Watoto CCT,  Shemasi Ester Mahagachi amewaasa waratibu na makatibu wa Ushirika wa mama wa kikristo Tanzania (UMAKI) Kugombea nafasi za Uongozi kwenye Uchaguzi ujao wa Serikali za mitaa na zile za Udiwani na Ubunge utakaofanyika mwaka ujao.

Bi. Ester ameutoa Wito huo wakati alipokuwa akifunga mafunzo ya Uongozi, Uundwaji na Usimamizi wa Vikundi vya akiba na mikopo kwa Waratibu wa Kanda na Makatibu wa Umaki toka Dayosisi 16 za kanisa Anglikana Tanzania waliokutana kunoana jijini Dodoma.

“wengi wetu tumepitia mafunzo mbalimbali na tuna zoefu katika uongozi Tunapoenda kwenye maeneo yetu kuongoza tusiishie tu kanisani twendeni tukachukue fomu za kugombe uongozi wa kijamii, si tunajua kuwa mwaka huu ni uchaguzi wa serikali za mitaa ambapo pia ni maandalizi kuelekea uchaguzi mkuu wa mwakani?” amesema na kuhoji,

Tuna nguvu na tuna uwezo wa kuongoza tukajitokeze, kugombea kwani siyo dhambi, kumbuka usipojitokeza wewe kugombea watajitokeza wengine na watakuongoza baada ya kuchaguliwa”, amesema

Aidha amesema “Nenda karekebeshe kumbukumbu zako kwenye daftari la mpiga kura lakini wakati ule wa uchaguzi nenda kapige kura maana usipoenda wewe wengine watamchagua mtu ambaye hukumuhitaji hata kama hana uwezo na atakuongoza utake usitake”,

 

Awali Mratibu wa Kanda ya Magaribi, Judith Kaigarula  wakati akisoma Risala mbele ya Mgeni Rasmi, mafunzo hayo yaliwashirikisha Waratibu wa kanda 4 za Kaskazini Mashariki, Kanda ya Ziwa, Kanda ya Kati na kanda ya Magaribi Pamoja na Makatibu wa Umaki wa Dayosisi 16 kati ya 28 za Bara na Visiwani.

Ambapo amesema mafunzo mengine waliyoyapata ni Pamoja na kuzitambua rasilimali zilizowazunguka makanisani na kisha kuzitumia kwa ajili ya maendeleo ya kanisa na watu wake.










Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG