BANDA MEDIA BLOG

KANISA LA ANGLIKANA TANZANIA LATOA MSAADA WA MAGADORO, VYAKULA VYA ZAIDI MILIION 18 KWA WAATHILIKA WA MAFURIKO MANYONI

 
 Askofu wa Dayosisi ya Rifty Valley mkoani Singida, John Lupaa akikabidhi msaada wa Godoro, Branket na Mahindi kilo 60, kwa mmoja wa wahanga wa mafuriko yaliyosababishwa na mvua zilizoambatana na upepo mkali, yaliyotokea mwezi januari mwaka huu katika kijiji cha sasajila wilayani Manyoni.

Katibu wa Umoja wa wanawake wa Kikristo Tanzania (UMAKI) Dkt, Ley Canon Margareth Ndonde akitoa msaada kwa mwanafunzi ambaye wazazi wake walikumbwa na kadhia hiyo




Katibu wa Umoja wa wanawake wa Kikristo Tanzania (UMAKI) Dkt, Ley Canon Margareth Ndonde, akitoa msaada huo kwa mmoja wa waathilika

Mke wa Askofu Devota Lupaa akitoa msaada kwa mmoaja wa waathilika hao

 (PICHA ZOTE NA JOHN BANDA)


Katibu wa Umoja wa wanawake wa Kikristo Tanzania (UMAKI) Dkt, Ley Canon Margareth Ndonde, akizungumza jambo kwenye Ugawaji wa Misaada hiyo.

              (PICHA ZOTE NA JOHN BANDA)

                                                            ............

                 NA JOHN BANDA, SINGIDA

KANISA Anglikana Tanzania, limetoa msaada wa Vyakula, Magodoro na Mabranketi yenye thamani ya Zaidi ya milioni 18 za Kitanzania kwa kaya Zaidi ya 100 zilizokumbwa na mafuriko januari kwaka huu katika Kijiji cha Sasajila kata ya chikuyu wilaya ya Manyoni Mkoani Singida.

Akiongea Julai 22,2024 nje ya kanisa la Mtakatifu Methew Anglikana Sasajila, mara baada ya kukabidhi Misaada hiyo Askofu wa Dayosisi ya Rifty Valley mkoani Singida, John Lupaa amesema kanisa anglikana Tanzania kwa Kushirikiana na Dayosisi hiyo wametoa msaada huo kwa wahanga waliokumbwa na mvua zilizoambatana na Upepo mkali.

Amesema Mvua hizo zilisababisha uhalibifu mkubwa wa mali za wakazi Zaidi 165, wanaotoka kaya 104 katika Kijiji cha Sasajila, kata ya Chikuyu wilayani humo ambapo Nyumba za makazi, Vyakula na mali nyingine vilihalibiwa na kuwafanya wakazi kukosa makazi.

“kigezo kilichotumika kuwapa misaada hii ni kutokana na watu hawa kukosa makazi na vyakula kutokana na nyumba, mazao waliyokuwa wamelima  kusombwa na maji wakati wa mvua hizo za mwezi januari mwaka huu”, amesema

Kwa Upande wake Katibu wa Umoja wa wanawake wa Kikristo Tanzania (UMAKI)  Dkt, Ley Canon Margareth Ndonde amesema moja ya kazi za kanisa ni kuwafikia watu wenye uhitaji, wakiwemo walikuombwa na Madhila mbalimbali kama hayo yaliyosababishwa Mvua za Upepo mkali.

“kanisa limetoa msaada wenye thamani ya sh. Milioni 18 tukijua msaada huo utawasogeza sehemu, maana wao hawakujitakia bali ni kutokana na majanga ya asili na kwamba wataendelea kuwaombea”, amesema Dkt. Ndonde aliyemwakilisha Katibu Mkuu wa kanisa Anglikana Tanzania, Mchungaji/ Canon Bethael Mlula

Mwenyekiti wa Kitongoji cha Weza B. Bonface Mahajile amesema msaada huo utatumika vizuri, kwa kuwa atahakikisha anawafuatilia wahanga 48, wanaotoka katika kitongoji chake ili kuhakikisha hakuna anayeuza au kutumia vibaya msaada huo uliotolewa na kanisa la Anglikana.

Nae Chapa Muganda mwenye asili ya kisukuma, akiongea kwa Kiswahili cha kubahatisha kutokana na kutokijua sawasawa na Anjelina Msangu wamelishukuru kanisa la Anglikana kwa kuwapa msaada huo ambapo chakula hicho kitawasogeza kwa Zaidi ya miazi miwili.

Mvua zilizoambatana na upepo zilisababisha mafuriko katika Mikoa ya Tanzania Kuanzia januari mwaka huu, Mpaka katikati ya Mwezi wa Nne ambapo yalisababisha maafa makubwa, yakiwemo ya watu kupoteza Maisha, Mali, vyakula na nyumba za makazi.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG