Sehemu ya wa wanafunzi waliopandishwa daraja la Ukristo kwa kuwekewa kipaimara na Askofu wa DCT, Dkt. Dickson Chilongani,
(PICHA ZOTE NA JOHN BANDA)
…………….
NA JOHN BANDA, DODOMA
KANONI Mstaafu, Hosea Chibago ambaye kwa sasa ametimiza
umri wa miaka 89 tangu kuzaliwa kwake, na ambaye amepata kuhudumu ndani ya kanisa
la Anglikana Tanzania, Dayosisi ya Central
Tanganyika (DCT) katika nafasi mbalimbali za uongozi tangu mwaka 1968 amesema miaka
michache ijayo kanisa hilo litakuwa tishio kiuchumi na kimaendelo hapa nchini.
Chibago ambaye mwaka 1968, alikuwa na cheo cha
kateksiti anasema hivi sasa kutokana na Ukomavu wa Wakrito wa DCT, walioanza
kujengwa tangu miaka ya nyuma Ambapo kanisa lilikuwa na mradi wa kutoa elimu ya kuwafunza kusoma na kuandika
uliojulikana kwa jina la TIMU, walipofaulu walipewa Biblia na kisha baadae kuwabatiza.
“wakati ule hasa huko vijijini watu wengi walikuwa
hawajui kusoma na kuandika hivyo kanisa likaja na mradi wa kuwasomesha ulioitwa
TIMU na walipojua kusoma na kuandika walipewa biblia na kuukubali ukristo wa
anglikana’, amesema
Mstaafu huyo ambaye mwaka 1977, aliwekewa mikono na
kuwa mchungaji Rasmi na baadae kuwa CANON cheo ambacho kilimsogeza katika ofisi
ya Askofu wa DCT na kuwa mshauri wake mpaka alipostaafu mwaka 2004, anasema kanisa
limekuwa na miradi mbalimbali ikiwemo ya ufugaji wa kuku, mbuzi, ng’ombe wa
maziwa, lakini pia utoaji wa Elimu na Afya kwa jamii kwa lengo la kujijenga kiuchumi
na kujiletea maendeleo.
Amesema kwa sasa kanisa linaelekea kwenye maendeleo
makubwa ya kiuchumi kwani hivi sasa baada ya DCT, kukamilisha na Kuzindua jengo
la Kitega uchumi la SAFINA lililopo kanisa kuu la Roho mtakatifa mwaka 2023, Askofu
aliyopo madarakani Dkt. Dicksoni Chilongani amekuwa mstari wa mbele kuhamasisha
ujengaji wa vitega uchumi katika maeneo ya mapareshi.
“ninachokiona miaka michache ijayo DCT hatashikika
kiuchumi na kimaenendeleo itatisha katika Madayosisi yote hapa Nchini”, amesema
Ameongeza kuwa Wachangaji ili waweze kufanya kazi ya
Mungu vizuri, katika kulichunga kanisa hutegemea sadaka ili waweze kujikimu
katika Maisha, lakini sadaka zimekuwa hazitoshelezi na pia huwezi kuwakamua
washirika Zaidi ya uwezo wao lakini kwa kuanzisha miradi itasaidia makanisa
kuwa na nguvu za kuhudumia watumishi vizauri, huku kazi ikisonga mbele kwa furaha
na amani.
ASKOFU DKT. CHILONGANI
Kwenye Kanisa la Saint Peter Parishi ya Kisasa likiungana
na Msamalia Mwema la Ilazo jijini Dodoma, julai 14,2024 Askofu Dicksoni
Chilongani amewawekea Mikono na kuwaingiza katika daraja la Ukrito, wakristo
84, wanaume na wanawake, ambapo baada ya huduma hiyo anayataka makundi ya kwaya
kuanza kujitafutia maeneo ya kuwekeza ili kuepuka kuomba michango kila wakati.
“kama ambavyo Parishi zimeanza kuwa na kasi ya kuweka
vitega uchumi katika maeneo ya makanisa yao kwa kujenga fremu za Biashara, vyoo
vya kisasa vya kulipia, naagiza hata makundi ya kwaya kuanza kutafuta maeneo ya
kuwekeza miradi yao ambayo itawasaidia kupata fedha za kujiendesha badala ya
kutegemea kuomba michango kila inapotokea safari za kihuduma’, amesema Dkt. Chilongani
Aidha Akofu huyo amesema anataka kanisa linalokuwa kiroho
na Kiuchumi.
“mwaka 2022 tulibatiza wakristo Elfu 13, mwaka 2023 tulibatiza elfu 18 leo nimewawekea
mikono 89 jana 300 bado naendelea na huduma hiyo haya yote yanatokana na kujitoa
kwetu kufanya uinjilisti,
Uinjilisti uende Pamoja na uwekezaji, kama
ninavyosema mara nyingi sitaki kanisa masikini, kanisa masikini haliwezi kutimiza
utume wake, tunataka kanisa linaloweza kutimiza utume kwa vyanzo vyake vya
ndani”, amesema na kuongeza
DCT. Ina jumala ya Parishi 300 zenye wachungaji 300
huku kukiwa na makanisa madagomadogo 1264, mwaka uliopita jumla ya walioingizwa
kwenye daraja la Ukristo, kwa kuwekewa kipaimara walikuwa 992 ambayo ni kasi
kubwa ya ukuaji wa kanisa hilo ambalo lina mpango miaka ijayo kwenda Ulaya
ambako kwa sasa kanisa linalegalega kwa
ajili ya kupeleka injili kwa kujigaramia lenyewe.