BANDA MEDIA BLOG

SHTGA YAWAINUA KIUCHUMI WANAWAKE WASUSI WA VIKAPU – NYANDA ZA JUU KUSINI.

 

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule akifurahia jambo pamoja na wanawake Wasusi wa Vikapu toka njombe, alipotembelea Banda la We Effect lililopo katika viwanja vya maonyesho ya  Nane-nane jijini humo.

                                              .................

         NA JOHN ISRAEL, NANE- NANE DODOMA


TAASISI ya Southern Highlands Tree Growers Association. (SHTGA) inayofanya shughuli  zake  Nyanda za Juu kusini mwa Tanzania yenye makao yake makuu  mkoani Njombe katika  jitihada zake kuboresha hali ya uchumi kwa vikundi wanachama wake inajuvunia kuwezesha zaidi ya wanawake 40 wasusi wa vikapu.

SHTGA Kupitia mradi wake unaofadhiliwa na Shirika la Kimataifa la Kimaendeleo la WE-EFFECT , Iimewawezesha wanawake wasusi wa vikapu wa nyanda za juu kusini  kwa kuwapatia mafunzo mbalimbali ya kuongeza ubora na thamani katika bidhaa hiyo ya vikapu mitindo vya mbalimbali

Mary Uswege (Meneja miradi – SHTGA  anesema Taasisi hiyo imekuwa ikitoa Elimu ya ujasiriamali na masoko ikiwa ni pamoja na kuwatafutia masoko yenye tija , ndani na nje ya nchi.Pia, kupitia mradi huo wanawake hao wamepata fursa ya kushiriki katika maonesho ya kimataifa ya kilimo (Nanenane :2024) yaliyofanyoka Kitaifa katika Viwanja vya Nanenane vilivyopo Nzuguni, Jijini Dodoma yalihusisha sekta mbalimbali ikiwemo Kilimo, Ufugaji na Uvuvi.Ikiwa ni fursa nzuri kwa wanawake hao kuweza kujifunza na kufahamiana na wadau mbalimbali wa sekta hizo, Sanjari na kupanua wigo wa masoko ya bidhaa zao.

Meneja miradi kutoka Taasisi ya SHTGA Bi. Mary Uswege anasema, mpaka sasa wameshaanza kugusa masoko ya Nje, kutokana na ubora wa bidhaa zao, Idadi kubwa ya wateja iliyowafikikia katika masoko ambayo wahusika waliona bidhaa zeo kwenye ukurasa  wao wa Instagram inayofahamika kama @fn_handmadebasket.

amesema Kupitia mafunzo yaliyotolewa kwa wanawake hao wameweza kusuka vikapu vyenye ubora wa hali ya juu katika mitindo mbalimbali yenye ladha na muonekano wa asili na ule wa kisasa vikiwemo vikapu vya kubebea kompyuta mpakato (Laptop bag), vikapu vya maua na urembo pamoja na mikoba ya kike, ambayo humpatia mtumiaji wa vikapu hivyo unadhifu wa kipekee.

Ameongeza kuwa, “kama SHTGA tunajivunia kuwawezesha wanawake hawa kutengeneza vikapu vyenye  ubora vinavyokidhi mahitaji ya soko la hapa Tanzania lakini pia la nje”,

 Ameeleza, shughuli hizi ni za kiutamaduni na endapo wakiulizwa wasusi hao, walivyopata ujuzi husema walifundishwa na Bibi, Mama na Shangazi zao. Hivyo; pamoja na Taasisi kuwaongezea maarifa hayo na kuwawezesha kupata kipato pia wanahakikisha utamaduni huo unatunzwa na kurithishwa vizazi na vizazi.

Aidha, amewapongeza wanawake hao, wasusi wa vikapu kwa ustadi wa kipekee katika kutengeneza vikapu hivyo.Na kuongeza kuwa, kwa sasa wanawake Zaidi ya 40 wananufaika na kupata kipato kutokana na kuuza vikapu kwa bei ya thelathini elfu hadi arobaini na tano elfu(30,000-45,000) kwa kila kikapu ikilinganishwa na bei ya awali kabla ya vikapu hivyo kuongezewa thamani ambapo kiliuzwa kwa  Elfu kumi hadi Elfu kumi na tano(10,000-15,000) kila kimoja abapo Shughuli hizo za uuzaji wa vikapu vimewawezesha wanawake hao kupata kipato na kuboresha maisha yao.

Ameongeza kuwa jamii kiujumla  wameweza kujenga nyumba ,kusomesha watoto, wamepata mitaji na kuwekeza katika shughuli nyingine ili kuongeza kipato kama vile, biashara na kilimo hivyo  kuongeza usalama wa chakula.

Bi. Mary Uswege (Meneja miradi – SHTGA) amehitimisha kwa kufafanua kuwa “ Wanawake  walionufaika chini ya mradi huu ni wale walio katika vikundi wanachama wa Muungano wa wakulima wa miti Nyanda za Juu Kusini.” 

Meneja Miradi wa taasisi ya SHTGA Mary Uswege akimuelezea Rc. Senyamule jambo kuhusu ususi wa vikapu bora unaofanywa na wanawake wa nyanda za juu kusini wanaoshiriki maonyesho ya Nanenane 2024 jijini Dodoma.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG