......................
NA JOHN BANDA, DODOMA
MAONYESHO ya Wakulima na Wafugaji ambayo yamekuwa
yakionyesha zana mbalimbali za Kilimo na Mifugo yamehitimishwa kitaifa hivi
karibuni na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan jijini Dodoma ambapo alitumia nafasi
hiyo kuzindua miradi mbalimbali ya sekta hizo muhimu hapa nchini
Katika maonyesho hayo yaliyofanyika katika
viwanja vya Nane-nane Nzuguni jijini humo, yalihusisha mashirika na makapuni mbalimbali
ya ndani na nje ya nchi kuonyesha vumbuzi na bunifu ambazo zikitumiwa kama
zilivyokusudiwa ni wazi kuwa taifa letu litapiga hatua za kimaendeleo katika
kila eneo hasa katika Mifugo na kilimo.
Ndani ya Maonyesho hayo Kumekuwa na Shirika
la Kimataifa la Maendeleo la WE EFFECT, lenye
makao yake makuu huko nchini Swiden ambalo linafanya kazi katika nchi Zaidi ya
20, katika mabara ya Asia, Latini Amerika na Africa Mashariki ambapo Ofisi za
kanda zipo Nairobi Nchini Kenya likiwa na uzoefu wa miaka 60, tangu lilipoanza shughuli
zake.
Meneja wa Shirika hilo Tanzania, Frank Adimba
anasema lengo kubwa la Shirika hilo ni
Kuondoa Umasikini kwa wakulima na makundi mengine kupitia vyama vya ushirika na
kwamba hadi sasa linafanya kazi na vyama Pamoja na taasisi 13 hapa nchini,
ambapo linajivunia kuwafikia watu laki 120 wanaojishghulisha na kilimo.
“hapa nchini tayari tunafanya kazi na
vyama vya ushirika 13, tukiwa tumewafikia wakulima laki moja na elfu ishirini (120,000)
huku asilimia 54 wakiwa ni wanawake”, amesema
Amesema kuwa malengo makubwa ni
kuhakikisha kuwa walengwa wanakuwa na Maisha bora Pamoja na haki ya upatikanaji
wa chakula (USALAMA WA CHAKULA) kwa kuwajengea uwezo kupitia Vyama vyao vya
ushirika.
Anasema katika vyama hivyo vya ushirika Pamoja
na taasisi za kiraia ambazo wanafanya nazo kazi mara nyingi zimekuwa zikilegzlega
kwenye uongozi, hasa kwenye kuwasaidia wakulima kufikia malengo, hivyo Shirika huwawezesha kuweka mifumo
thabiti ya Uongozi, Sera Bora kwa ajili ya kuhakikisha kuwa wanasima kitaasisi.
Anasema Lengo lingene ni kuwa wanahakikisha
wanaimarisha mifumo ya Chakula, kupitia Kilimo kwani wadau wao ni wakulima kwa
kuanzia Uzalishaji, Usindikaji mpaka uuzaji wa bidhaa mbalimbali ndani ya
mnyororo wa thamani.
Meneja huyo Anesema shirika linawajengea
uwezo wakulima wa kuhakikisha wanakuwa na uwezo wa kujenga nyumba bora za
kisasa, kwani si busara Mkulima
akazilisha na kuuza huku akawa bado anaishi kwenye nyumba isiyo na hadhi.
WE EFFECT kupitia Programu yake ya Ujenzi
wa nyumba bora vijijini kwa sasa linajivunia Zaidi ya nyumba 5000 zilizojengwa na
wakulima wa Tanzania kutokana na kuchangishana wakichagizwa na huduma ndogo ya
za kifedha
“tunawafundisha kupitia mkondo wa huduma
ndogo za kifedha, wanafikia hatua ya kuwekeza na kuwezeshana kwa kuchangishana
kiasi cha kufikia hatua ya kujenga nyumba ambapo sasa tunajivunia nyumba bora
5000 tayari zimeshajengwa na wakulima hapa tanzania”, amesema
USHIRIKA
Aidha Meneja Adimba amewataka Wakulima na
Makundi mengine kujiiunga kwenye Vyama vya ushirika ili wakatengeneze Nguvu na
Sauti ya Pamoja ambayo itawafanya kusikika kama ilivyo Nchii Kenya ambako
makundi mbalimbali yakiwemo Bodaboda, Mbogamboga, madereva wa matatu na mengine
mengi yanaungana Pamoja.
“ushirika unawaleta watu Pamoja, wanakuwa
na nguvu na sauti ya Pamoja ya kuweza kueleza mambo yao yakasikika lakini pia
kuongeza uzalishaji, kwani mkono mmoja haupigi makofi,
Pia ukitaka kwenda haraka nenda peke yako,
lakini ukitaka kwenda mbali kwa uhakika nenda na wenzako mtafika salama lazima
mkiwa kwenye ushirika mtakidhi mahitaji ya soko”, amesema na kuongeza
Ameongeza kuwa “mkiwa Pamoja mtapanga bei
ya Pamoja Pamoja na kupata soko la uhakika kunakosababishwa na kuuza kwa Pamoja”,
pia amesema Benki Kuu ya Ushirika ya nchini
Kenya ndiyo inayoongoza nchini humo kwani wakulima wote wana hisa hivyo huweka
na kukopa kwa ajili ya kuendeza fani yao, hivyo kwa Tanzania amesikia hivi
karibu kutazinduliwa Benki ya KCBL ambayo amesema itakuwa mkombozi kwa wakulima
na makundi mengine yatakayokuwa na hisa.
Shirika hilo linawezesha vyama vya
ushirika vinavyotoka na wakulima, wafugaji, walinaji wa asali, wasusi wa
vikapu, wakusanya maziwa na kuyasindika na kuyauza, wachongaji wa zana za
mikono Pamoja na wengine mengi.