Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma SACP Anania Amo akizungumza na waandishi wa habari leo Agosti 13,2024 jijini Dodoma
NA JOHN BANDA, DODOMA
WAANDISHI wa Habari walibana kwa maswali Jeshi la Polisi mkoni Dodoma kuhusu kifo cha mwanamuziki wa Bongo Fleva Josephas Michael Maarufu Man'dojo lenyewe latoa ufafanuzi huku likitoa onyo kwa wanaojichukulia sheria mkononi.
Man'dojo ambaye enzi za uhai wake alipata
kutamba na vibao kadhaa kikiwemo Nikupe Nini Honey akishirikiana na Domokaya, Taarifa za Kifo Chake zilizagaa
kwenye Mitaandao mbalimbali ya kijamii Pamoja na Baadhi ya vyombo vya Habari Agosti
11, mwaka huu,
Akitoa Ufafanuzi hii leo agosti 13,2024 Kaimu Kamanda wa
Polisi mkoa wa Dodoma, Anania Amo mbele ya Waandishi wa Habari amesema Majira
ya saa 6 mchana wa siku hiyo Mandojo alipoteza Maisha wakati alipokuwa
akipatiwa matibabu katika hospital ya Rufaa ya Mkoa huo.
Akifafanua Zaidi amesema saa 11 alfajiri
ya Siku hiyo Mandojo ambaye ni mkazi wa Nzuguni B, Jijini humo alikutwa katika
moja ya chumba Kilichopo ndani uzio wa Kanisa la Rc. Parokia ya Watakatifu Wote ambapo mlinzi
alishtushwa na sauti za Mbwa aliyekuwa akimbwekea na ndipo akaingia chumbani
humo.
“mlinzi baada ya kusikia mbwa akibweka
ndipo alipoenda kuangalia kuna nini ndipo alipogundua kuna mtu ndani ya chumba
hicho ambapo akapiga kelele kuita watu wamsaidie ambapo waumini waliokuwa
wanaingia ibadani misa ya kwanza siku ya Jumapili wakafika wakaanza
kumshambulia Mandojo kwa Pamoja”, amesema
Aidha Kaimu Kamanda huyo amesema jeshi
hilo lina mshikilia Kwa Mahojiano kuhusiana na Tukio hilo Mlinzi huyo Rafael
Keneth.
Kaimu huyo ambaye ni Kamishna msaidizi wa
Jeshi la Polisi amesema Watu wengine Wawili Franco Filibert (29) Muhaya na Ramadhan
Abeid (27) Mzgua wameuawa kwa kupigwa katika maeneo mbalimbali ya miili yao na
kisha wakachomwa moto ndani ya Gari yao huko Ibihwa wilayani Bahi.
Amesema watu hao waliotoka Dodoma mjini
walifika ibihwa wakielekea katika kitongoji cha Juhudi kupeleka Token za mchezo wa kubahatisha
majira ya saa 4 usiku wa Agosti 8, 2024 wakiwa na gari yenye namba za usajili T 583
BEW aina ya Toyota Crester ambapo hawakuendelea na safari kutokana na barabara
kutopitika ikabidi wamtume wenzao kupeleka tokeni hizo kwa Bodaboda.
“wapita njia walilitilia mashaka gari
hilo kutokana na kuegeshwa katika eneo hilo kwa Muda mrefu, ndipo wakaitana na
kuanza kuwashambulia kisha kulichoma gari hilo huku watu hao wakiwa ndani hali
iliyosababisha kifo chao miili yao imehifadhiwa katika chumba cha kuhfadhia
maiti katika hospital ya wilaya ya Bahi”, amesema
Baada ya taarifa hizo maswali ya
waandishi wa Habari yakaibuka, wakita kujua Kwanini Afisa Mtedaji huko Ibihwa
alizuia Gari ambalo lilichomwa moto lisipigwe Picha lakini pia Matukio ya
wananchi kujichulia sheria Mkono yatakoma lini lakini pia jeshi hilo lina
mkakati gani kwa ajili ya Usalama wa Raia na mali zao maana mara nyingi askari
wa Doria wamekuwa wakifika kwenye mitaa kutokana na matukio?
Kaimu Amo akijibu amesema Jeshi hilo
halikumuagiza Mtendaji huyo kuzuia waandishi wasifanye kazi yao katika eneo la
tukio, kuhusu wananchi kujichukulia sheria Mkoni amesema jeshi hilo limekuwa
likipita katika taasisi za dini, mashuleni na kwenye mikusanyiko kutoa elimu na
kuhusu Doria “tuna askari wachache hivyo hawawezi kuwa kila sehemu kwa wakati
mmoja hivyo wananchi wahakikishe wanatoa ushirikiano kwa kuanza kujilinda wao
kabla ya polisi kufika.