BANDA MEDIA BLOG

ALIYEWAHI KUKOSOA VIONGOZI WA AFRICA KUNG'ANG'ANIA MADARAKA AWANIA MHURA WA 7

 .

Raia wa Uganda walio na umri wa chini ya miaka 40 - na ambao ni zaidi ya robo tatu ya watu - wamemfahamu rais mmoja tu.

Yoweri Museveni alinyakua wadhifa huo wa juu mwaka 1986 kufuatia uasi wa kutumia silaha na akiwa na umri wa miaka 81, haonyeshi dalili za kuwachia.

Wakati wake wa uongozi umeambatana na kipindi kirefu cha amani na maendeleo makubwa, ambayo wengi wanashukuru. Lakini wakosoaji wake wanasema anang'ang'ania madaraka kupitia mchanganyiko wa kuwatenga wapinzani na kuzitumia vibaya taasisi huru.

"Hatuamini katika ukomo wa mihula [ya urais]," aliwahi kuiambia BBC, akiutetea wadhfa wake baada kushinda uchaguzi wa tano.

Mwaka mmoja baadaye, ukomo wa umri wa mgombea urais uliondolewa - na kufungua njia, kwa Museveni kuwa rais wa maisha.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG