BANDA MEDIA BLOG

WACHIMBA MADINI UJENZI ZAIDI 100 DODOMA WALALAMIKIA ENEO LAO KUPIMWA KINYEMELA, DIWANI MPONYAMILI AINGILIA KATI

DIWANI wa kata ya Iyumbu Jijini Dodoma Sadiki Mponyamili ametembelea na kujionea shuhuli zinazofanywa na Wanakikundi cha Wachimba kokoto cha NZINJE IYUMBU na kubaini eneo lao la Leseni limepimwa viwanja huku wakifungiwa mashine yao ya kukusanyia Ushuru (POS).

Mwenyekiti wa Mtaa wa Iyumbu Nasson Lugunyale amesema kutoakana na hali hiyo kumesababisha familia nyingi kuishi Maisha ya Taabu kwani wengi wao walitegemea shuhuli hiyo kutunza familia zao kwa zaidi ya miaka 43.

“inashangaza sana wamefungiwa kutofanya kazi zao za uchimbaj wa madini wakati leseni yao bado inasoma, ambapo sasa hali za familia za wachimbaji hao zaidi ya 100 ni tete kwani wanashindwa hata kuwalipia ada Watoto wao pamoja na maendeleo mengine” amesema

Diwani Mponyamilia akichapisha kwenye ukurasa wake wa Facebook ameandika,  “Leo nimetembelea na kuwasikiliza Wana kikundi wanaojihusisha uchimbaji madini ujenzi (kokoto,mawe)... KIKUNDI CHA NZINJE IYUMBU 

Nimesikiliza changamoto zao Ili kuona ufumbuzi zaidi.

Moja kati ya changamoto yao ni kuwa mashine Yao ya kukata ushuru (POS) imefungwa , mashine hiyo ilifungwa huku kukiwa na madai kuwa hawaruhusiwi kuendesha shughuli hiyo ya uchimbaji madini ujenzi lkn pia nmeweza kujua kwamba wanayo LESENI inayofanya kazi (active licence up to 2027),huku kero Yao kubwa kwann wamefungiwa mashine ambayo ingesaidia kupata mapato serikalini na kwamba jambo hili nimelipokea kwa utatuzi zaidi.....

Lakini pia wameibua hoja ya Eneo Hilo kudai limepimwa kinyemela bila wao kuhusishwa na kwamba Eneo Hilo pamoja na shughuli ile lkn ni Eneo ambalo wamekuwa na shughuli hyo tangu mwaka 1983 na Kisha 2013 wakaweza kupata LESENI Eneo Hilo,nimeahidi kulifanyia kazi

Mwisho wamefurahi kuona kiongozi wao amewatembelea kwani haikuwahi kutokea kiongozi wao kwenda Eneo lao la kazi na kuweza kuwasikiliza, zaidi wamekuwa wakiwasilisha tu changamoto zao serikali za mtaa... ",ameandika Mponyamili



Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG