BANDA MEDIA BLOG

KIKWETE AKUTANA NA MAALIMU SEIF IKULU JIJINI DAR.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete wa Tanzania amefanya mazungumzo na makamu wa rais wa kwanza kisiwani Zanzibar ambaye ndiye mgombea Urais kupitia tiketi ya chama cha upinzani (CUF) Maalim Seif katika Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Hatua hiyo inajiri wakati ambapo kuna mkwamo wa kisiasa kisiwani humo baada ya Tume ya Uchaguzi(ZEC) kufuta matokeo ya uchaguzi uliofanyika .
Hatahivyo mwandishi wetu aliyezungumza na mkurugenzi wa maswala ya mawasiliano katika chama cha CUF amesema kuwa hakuna lolote la muhimu lililoafikiwa isipokuwa 'mazungumzo ya kawaida'.
Amesema kuwa wamehuzunika baada ya kubaini kuwa rais Jakaya Kikwete anakamilisha muhula wake wa uongozi hapo kesho.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG