BANDA MEDIA BLOG

MH. KASSIM MAJALIWA NDIYE WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

Hatimaye kitendawili kimeteguliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli baada ya kumteua Mh. Kassim Majaliwa Mbunge wa Ruangwa mkoa wa Lindi  na Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu Tamisemi anayeshughulia elimu kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Akitangaza jina hilo Spika wa Bunge Mh. Job Ndugai amewaeleza wabunge kuwa kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inampa rais kuteua jina la Waziri Mkuu na kuliwasilisha bungeni kwa ajili ya kuthibitishwa na wabunge
Hivyo bunge litamthibitisha rasmi na kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Fullshangwe na kikosi chake chote kimatakia Mh. Waziri Mkuu Mteule  Kassim Majaliwa afya njema na mafanikio katika majukumu yake mapya.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG