Na Tiganya Vincent – MAELEZO
……………………………………….
Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linaendelea na kikao chake mjini Dodoma kwa Spika wa Bunge hilo Mheshimiwa Job Ndugai kuendelea kuwaapisha Wabunge waliosalia.
Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linaendelea na kikao chake mjini Dodoma kwa Spika wa Bunge hilo Mheshimiwa Job Ndugai kuendelea kuwaapisha Wabunge waliosalia.
Wakati zoezi hilo likiendelea ,shauku kubwa ya Waheshimiwa Wabunge na Watanzania ni kusubiri jina la atakayekuwa Waziri Mkuu.
Jina la Waziri Mkuu ajae
linatarajiwa kujulikana leo na hatimaye kupigiwa kura na wabunge mara
baada ya Spika kumtangaza rasmi kama mteule wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania kushika wadhifa huo.
Mara baada ya zoezi la kupitishwa
kwa jina la Waziri Mkuu kupitishwa na Bunge Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli atamwapisha mjini Dodoma.
Waziri Mkuu atakaye teuliwa na Mheshimiwa Rais atakuwa ni wa 11 kushika wadhifa huo tangu mwaka 1961.
Mawaziri Wakuu waliowahi kushika
nafasi hiyo ni pamoja na Mwalimu Julius Kambarage Nyerere( 1961-1962),
Mzee Rashid Mfaume Kawawa(1962,1972-1977),Edward Moringe
Sokoine(1977-1980,1983-1984), Cleopa David Msuya 1980-1983,1994-1995),
Dk. Salim Ahmed Salim 1984-1985), Joseph Sinde Warioba (1985-1990), John
Malecela (1990-1994), Fredrick Sumaye(1995-2005),Edward Lowassa
(2005-2008) na Mizengo Pinda (2008-2015)
Tags
Bunge
