 |
| Mchezaji wa Dom City akionyesha uwezo wake wa kumiliki Mpira mbele ya wachezaji wa Fire Stone. |
|
 |
Na John Banda,Dodoma
MWAMUZI
Salehe Mang’ola amenusurika kuchezea kichapo kutoka kwa wanaohisiwa kuwa
mashabiki wa timu ya Fire Stone kutokana na kutoridhishwa na uamuzi wake katika
mchezo wa kombe la Ng’ombe.
|
 |
Mchezaji
wa Dom City ya Nzuguni Bonface Mjerwa akimzidi ujanja Mlinzi wa Fire
Stone na kufanikiwa kupata goli kwa kumvisha Kanzu mlinda mlango wa timu
hiyo.
Tukio hilo
ambalo lilitokea juzi katika uwanja wa Mbuyuni Nzuguni manispaa ya Dodoma
wakati timu hiyo ikipambana na Dom City ya nzuguni.
Ilikuwa hivi
mara baada ya kupuliza filimbi ya kumaliza pambano hilo wanaohisiwa kuwa ni
mashabiki wa Fire Stone walianza kumfukuza mwamuzi huyo ambaye alitimua mbio hadi katika nyumba zilizopo
jirani na uwanja huo.
Mwamuzi huyo
mara baada ya kufika katika nyumba hiyo aliingia ndani na kujifungia hali
iliyowafanya mashabiki wa timu hiyo kubaki nje wakiwa wanashangaa tu.
|
 |
| Mpira uliopigwa na Mshambulizi Bonface Mjerwa ukiwa umechana nyavu kutokana na shuti kali |
Mwamuzi
huyo
alikaa ndani ya nyumba hiyo kwa zaidi ya dakika 40 akisubiria mashabiki
hao
waondoke,ambapo mashabiki hao waliondoka huku hasira zao zikiishia
kung'oa na kuvunja milingoti ya magoli uwanjani hapo, ndipo alipopata
nafasi kuondoka.
Hata
hivyo mwamuzi huyo mkongwe alipotakiwa kuzungumzia tukio hilo aligoma
kuongea kwa madai kuwa yeye siyo msemaji wa mchezo huo
Katika
mpambano
huo wa nusu fainali ya kombe la ng'ombe, Fire Stone ilikubali kipigo
cha bao 1-0 kutoka kwa Dom City iliyojihakikishia kuingia fainali.
mwisho
 |
| Mfungaji wa Bao pekee la Dom City akagalagala baada ya kukatwa na mabeki wa timu ya Fire Stone wakati hana Mpira |
 |
| vita ya soka kwenye mchezo huo |
 |
| Mwanzo wa kumzonga Mwamuzi |
 |
| Wachezaji wa timu za Fire Stone na Dom City wakimzonga mwamuzi baada ya wachezaji wa timu hizo kupigana |
 |
| Mfungaji wa Goli akitolewa nje kwa kadi nyekundu baada ya Mwamuzi kudanganywa na wachezaji wa Fire Stone |
 |
| Mashabiki wanaodhaniwa ni wa timu ya Fire Stone wakimvamia Mwamuzi Saleh Mang'ola mara baada ya filimbi ya mwisho ya mchezo huo |
 |
Mwamuzi huyo Saleh Mang'ola akaamua kutimua Mbio ili kujiokoa na kipigo toka kwa mashabiki hao mpaka ndani ya nyumba iliyokuwa jirani na Uwanja huo
 |
| Mwamuzi akichungulia kwa Mbali kama wabaya wake wameondoka |
|