Mvua ya gharika mpya inatishia
kuchochea maafa zaidi katika maeneo kadhaa ya Ulaya, yakiwemo maeneo
yaliyoathiriwa vibaya na mafuriko.
Mvua ya gharika Frank, inatarajiwa
kuanza jana jioni, huku maeneo ya Cumbria na kusini na kati ya
Scotland yakiwa hatarini.
Kumekuwepo na tahadhari tisa za
mafuriko, yakimaanisha hatari kwa maisha ya watu na wanyama
Uingereza, Wales hususan katikati ya York ambayo yameathiriwa vibaya
na mafuriko jumamosi.
Waziri Mkuu wa Uingereza David
Cameron ametetea matumizi ya serikali yake katika kukabiliana na
mafuriko baada ya madhara kutokea kaskazini mwa Uingereza.
Tags
KIMATAIFA

