Mahmoud Ahmad Arusha
Wakazi wa Arusha na Madereva wa
Daladala wameiomba serikali kuikarabati Stand ya daladala iliyopo
Samunge kwani ipo kwenye hali mbaya hususani kipindi hiki cha mvua huku
pia wakilalamikia msongamano wa magari kwenye lango la kuingilia Stand
hiyo hali inayoleleta usumbufu kwa wapita kwa miguu.
…………………………………….
Wakazi wa Arusha na Madereva wa
Daladala wameiomba serikali kuikarabati Stand ya daladala iliyopo
Samunge kwani ipo kwenye hali mbaya hususani kipindi hiki cha mvua huku
pia wakilalamikia msongamano wa magari kwenye lango la kuingilia Stand
hiyo hali inayoleleta usumbufu kwa wapita kwa miguu.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti
wakazi hao wamesema kuwa kumekuwa na hali mbaya wakati wa kupanda
magari hayo hususani kipindi hichi cha mvua na kuwataka watendaji wa
serikali na madiwani kuliangalia hilo ikiwemo kuweka moramu,na vibanda
sanjari na kuiboresha Stand hiyo.
Mkazi wa Kata ya Muriet Agnes
John alisema kuwa kumekuwa na usumbufu kwa nyakati tofauti kwenye stand
hiyo kiasi imekuwa Adha kwa wakazi wanaokwenda kupata huduma kwenye
stand hiyo huku akizitaka mamlaka husika kuliangalia suala la uboreshaji
wa stand hiyo.
“Jamani hebu tizameni stand hii
kwa ukaribu angalia hata sehemu za kupumzikia wanaokuja kupanda basi au
wanaosubiria jamaa zao kutoka eneo moja kwenda jingine ni shida hakuna
maeneo hayo ni msongamano wa magari bila ya mpangilio haya yanakwenda
wapi tunaomba mamlaka ziangilie hili”
Kwa upande wake Mkurugenzi wa
jiji Juma Idd yeye hakuweza kupatikana kwa simu yake ya mkononi na
gazeti hili linaendelea kumtafuta ilikulitolea majibu suala hilo ila kwa
upande wake Meya wa jiji la Arusha Kalist Lazaro alipopigiwa simu na
gazeti hili ilikujua baraza lake analoliongoza kama limepanga nini
kuhusu Stand hiyo alijibu kuwa yupo kwenye kikao cha elimu na kukata
simu yake ya mkononi bila maelezo.
Gazeti hili pia likaongea na
mmoja wa madereva wa Dala dala Abdallah Mwarabu alisema kuwa wamekuwa
wakifanyakazi kwenye mazingira magumu katika stand hiyo ikiwemo nyakati
za jioni kwani ndani ya Stand Taa zilizopo hazitoshelezi na zinawaweka
abiria kwenye wakati mgumu hivyo wamekuwa wakipakia nje ya stand hiyo.
Hali ya Stand hiyo ya daladala
iliyopo kwenye eneo la Samunge kata ya Levolosi imekuwa mbaya hususa
kwenye upitishaji wa maji wakati wa mvua hali inayoleta usumbufu kwa
abiria,huku kumekuwa hakuna sehemu ya abiria kupumzikia au kujikinga na
mvua wakati wakingojea usafiri kwenye stand hiyo
Tags
HABARI KITAIFA