Muonekano
wa kivuko cha MV. Malagarasi kilichopo katika eneo la Ilagala mkoani
Kigoma. Kivuko hicho kina uwezo wa kubeba abiria 100, magari sita na
tani 50 kwa wakati mmoja.
Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (wa tatu
kushoto), akipata maelezo ya kivuko cha MV. Malagarasi kutoka kwa
Msimamizi wa Kivuko hicho kabla ya kukikagua. Kulia ni Meneja wa Wakala
wa Barabara nchini (TANROADS), mkoani kigoma Eng. Narcis Choma na Wa
pili kushoto ni Mbunge wa Kigoma Mjini Mhe. Zitto Kabwe.
Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akishuka
katika Kivuko cha MV. Malagarasi mara baada ya kukikagua na kuona namna
ya kivuko hicho kinavyofanya kazi.
Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (wa pili
kulia), akioneshwa vifaa vya uokoaji katika kivuko cha MV. Malagarasi.
Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (kushoto)
akijadiliana jambo na mmoja wa abiria wa Kivuko cha MV. Malagarasi.
Meneja
wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS, mkoani kigoma Eng. Narcis Choma
(wa tatu kushoto) akimuonesha Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
Profesa Makame Mbarawa (wa tatu kulia), barabara ya Simbo-Kalya yenye
urefu wa zaidi ya Km 200 Kusini mwa Ziwa Tanganyika itakayoanza kujengwa
hivi karibuni wilayani Uvinza mkoani Kigoma.