BANDA MEDIA BLOG

WANAOHUJUMU VIPANDO PEMBA KUKAMATWA NA KUFIKISHWA KATIKA VYOMBO VYA SHERIA


indexNa Masanja Mabula – PEMBA .
JESHI la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba limeagizwa kuwasaka na kuhakikisha wahusika wote wa matukio ya kuhujumu vipando wanakamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria.
Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Mkoa huo ,Omar Khamis Othman  baada ya kuendelea kutokea kwa vitendo vya hujuma katika mashamba ya baadhi ya wananchi katika Mkoa huo.
Amesema vitendo hivyo ambavyo vinafanywa na watu wasiojulikana vinachangia umaskini kwa wamiliki wa mashamba jambo ambalo  halikubaliki na kwamba serikali ya Mkoa imelaani vikali kwani vinakwenda kinyume na Haki za binadamu.
Akizungumza baada  ya kukagua mashamba ya mihogo na migomba yaliyohujumiwa huko Tumbe Wilaya ya Micheweni , ambako mashamba matano yenye ukubwa wa eka tano likiwemo la Sheha wa Shehia ya Tumbe Magharibi wamehujumiwa na watu wasiojulikana.
“Vitendo hivi haviwezi kuvumiliwa , hakikisheni kwamba wahusika wanasakwa na wanakamatwa na kisha kufikishwa katika vyombo vya sheria ”alisema .
Mapema Mkuu wa Wilaya ya Michewenia Abeid Juma Ali amesema hujuma hizo ni za makusudi na zimepangwa na watu waliondaliwa kuhujumu mali za watu wengine , ambapo amewataka wananchi kutochukua sheria mikononi mwao.
Amesema pamoja na kwamba hujuma hizo zinaathiri sana juhudi zoa za kujikomboa na umaskini , ni vyema wananchi kuwasilisha malalamiko sehemu husika na sio kujichukulia sheria mikononi .
“Hivi ni vitendo ambavyo vinanyesha kama ni vya kupangwa , hivyo nawaomba sana wananchi kutochukua sheria mikononi mwao bali wafikishe malalamiko yao Serikali ili yafanyiwe kazi kwa mujibu wa sheria ”alisisitiza.
Naye  sheha wa Shehia ya Tumbe Magharibi Massoud Khamis Kirendo amesema kuwa amesikitishwa sana na vitendo hivyo ambavyo vimefanywa na watu hao wasio julikana.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG