BANDA MEDIA BLOG

MAZOEZI MAKALI YANAENDELEA KATIKA KAMBI YA SUPER D COACH UHURU GYM KARIAKOO


Mabondia Faraji Sayuni kushoto na Hassani Kiwale wakioneshana umwamba wa kutupiana makonde wakati wa mazoezi yao yanayoendelea katika kambi ya Super D Coach Uhuru GYM Kariakoo mabondia wote hao watapanda ulingoni Agosti 8 katika ukumbi wa kobelo pub manzese Dar Es salaam Picha na SUPER D BOXING NEWS

 Bondia Hassani Kiwale kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Faraji Sayuni wakati wa mazoezi yao yaliyofanyika katika kambi ya Super D Coach Uhuru GYM Kariakoo Dar es salaam mabonda hao watapanda ulingoni Agosti 8 kuwakabili wapinzani wao katika ukumbi wa Kobelo Pub Manzese Dar Es salaam Picha na SUPER D BOXING NEWS
…………………………………………………………………………..
Na Mwandishi Wetu
MPAMBANO wa ubingwa wa taifa wa Kg 57 utagombaniwa na mabondia Kaisi Rashid na Faraji Sayuni siku ya Agostin 8 katika ukumbi wa Kobelo Pub Manzese Dar Es Salaam ,  Mpambano huo wa raundi kumi za ubingwa umeratibiwa na Promot Miraji Uliza ambapo kutakuwa na mapambano mengine mbalimbali ya mchezo wa masumbwi nchini Mabondia wengine watakaopanda siku hiyo ni Abdallah Pazi atakaezipiga na Said Mkone wakati Godrack Mrema atakumbana na Hassani Kiwale wakati Omari Uliza atazipiga na Bruno Fadhili na Said Jelemi atamkabili Azizi Kondo na Saleh Mkalekwa atacheza na Salum Ngula huku  Azizi Uliza akicheza  na Mohamed Matimbwa

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG