Ofisi ya Msajili wa Vyama
vya Siasa nchini Leo imekamilisha zoezi la kuhakiki vyama vya siasa 21
kwa upande wa Tanzania Bara . Zoezi la uhakiki wa vyama vya Siasa
visiwani Zanzibar litaanza Julai 11 mwaka huu.
Uhakiki wa Vyama utafanyika katika Ofisi za Vyama zilizopo
Zanzibar kwa maana ya Unguja na Pemba, zoezi hilo litajumuisha uhakiki
wa idadi ya wanachama ambao Chama cha Siasa kinapaswa kuwa nao kwa
mujibu wa masharti yalipo kwenye Sheria ya Vyama vya Siasa yam waka
1992.Ikumbukwe kuwa ,zoezi hili ni moja kati ya shughuli za kawaida za Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ambalo hufanyika maramoja kila mwaka likilenga kufahamu utekelezaji wa masharti na matakwa ya sheria ya vyama vya siasa.
Tags
SIASA