BANDA MEDIA BLOG

SPIKA NDUGAI ATUA DODOMA AAHIDI KUMALIZA MIGOMO YA WABUNGE WA UKAWA BUNGENI


Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Job Ndugai Akishuka kwenye ndege alipowasili mjini Dodoma akitokea jijini Dar es salaam alikorejea hivi karibuni akitoke nchini India alikokuwa akitibiwa Takribani miezi 3 iliyopita.
Akisalimiana na watu mbalimbali waliofika kumpoke uwanjani hapo wakiwemo waandishi wa habari

Ndugai akizungumza na wafanyakazi wa ofisi ya Bunge katika uwanja wa ndege wa Dodoma alipofika akitokea Jijini Dar es laam IMEANDALIWA NA BANDA BLOG
Spika wa Bunge Job Ndugai akielekeza jambo wakati alipokuwa akiongea na waandishi wa habari hawapo pichani, katika chumba cha kupumzika cha uwanja wa ndege wa Dodoma jana, Kushoto ni Mke wake Dkt. Fatma Mghana

Spika akisaini kitabu cha wageni uwanjani hapo

Akimshukuru Mke wake Dkt, Fatma Mgana kutokana na kujitoa kumhudumia wakati alipokuwa akitibiwa Nchini India


Na John Banda,Dodoma
SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Job Ndugai amehamia rasmi Dodoma huku akiahidi kulitafutia ufumbuzi  suala  la wabunge wa Ukawa kususia vikao vya bunge.
Kauli hiyo aliitoa jana,Mjini hapa alipowasili katika uwanja wa Ndege wa Dodoma akitokea Jijini Dar es Salaam ambapo awali alikuwa nchini India kwa Matibabu.
Alisema jambo linalomuumiza kichwa ni wabunge kutosalimiana pamoja na kutoshirikiana katika mambo  mbalimbali hivyo kuahidi kulishughulikia kwa kukaa pamoja na pande zote.
 “Tatizo langu mimi ningependa tuelewane na wabunge, ilifikia wakati mahusiano ya wabunge wa pande hizi mbili yalikuwa mabaya mno , kama mnakumbuka sehemu kubwa ya kipindi kile cha  mwezi wa Ramadhani ilifika mahali hata mtu fulani akitengeneza futari watu wa upande fulani hawawezi kwenda  kula futari wabunge ni timu moja lazima tushirikiane’’alisema
Uendeshaji wa Bunge na wabunge kukosea kanuni
Alisema katika mabunge mengine kila bunge jipya la zamani linapomalizia muda wake linapitia kanuni mpya na bunge linalokuja watu wapya linakuta kanuni zilizorekebishwa na walioondoka
“Sisi mwaka 2007 tulirekebisha tuliokuwa bungeni sio jambo zuri kwani unatengeneza sheria wakati wewe ni mchezaji, sheria zinatakiwa kutengenezwa na watu wengine halafu wachezaji wanaenda kucheza kwa kutumia sheria zilizotengenezwa” alisema
Alisema kwa utaratibu uliopo kanuni zipo, spika na wenzake wanatakiwa kutilia mkazo na wabunge wazielewe na kuzitekeleza wameshatoa semina na makongamano ya kutosha na wako tayari kuelimisha wabunge kama kuna haja ya kufanya hivyo.
“Kama kuna kanuni ambazo wabunge wanaona zina matatizo makubwa, tunao muda wa kupendekeza hivyo kwa spika na tunayo kamati maalum tunaita kamati ya kanuni ambayo ikipokea mapendekezo ya namna hiyo inafanyiwa kazi yakishafanyiwa kazi huwa lazima mapendekezo hayo yaende kwenye bunge zima ili wabunge wote wakubali hiki kibadilike hiki hakikuwepo kiingizwe au hiki kitoke” alisema
KUHAMIA DODOMA
Kuhusina na kuhamia Dodoma,Ndugai alisema ofisi yake imeishahamia rasmi huku wale waliokuwa wakifanya kazi Dar es salaam nao watajiunga katika siku za hivi karibuni.
‘’Wote tumekuja Dodoma tulikuwa na ofisi ndogo Dar wote watakuja Dodoma watabaki wachache tu kwa ajili ya suala la afya pamoja na wale wanaotaka kusafiri’’alisema
mwisho



Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG