BANDA MEDIA BLOG

SASA MAJI KULIPIWA KABLA KAMA LUKU, SHIRIKA LISILO LA KISERIKALI LA ICS LAONYESHA MITA YA MAJI YA MALIPO YA KABLA

Meneja Mauzo wa Shirika lisilo la kiserikali la ICS linalotekeleza mradi wa maji wa Maganzo wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga Abraham Mwanyamaki akichangia jambo wakati alipokuwa akiuelezea  umuhimu wa malipo ya kabla ya kutumia maji kwenye kongano la mwaka la maji lilofanyika mjini Dodoma likiandaliwa na Jumuia ya wasambaza maji ya  ATAWAS

Mhandisi Tarcisius Opta anayesimamia Mradi wa Maji wa Maganzo wilayani Kishapu Mkoa wa Shinyanga akimuelekeza Katibu Tawala msaidizi katika huduma za maji wa mkoa wa Dodoma Mathayo Athuman  mwenye suti nyeusi,  jinsi ya kuwasha Mita maji ya malipo ya kabla wakati alipotembelea Banda la maonyesho la ICS lenye makao yake makuu nchini Uholanzi  linalojishuhulisha na miradi ya maji vijijni [PICHA NA JOHN BANDA]

Mwenyekiti Jumuia ya wasambaza maji mijini na vijijini ya ATAWAS  Mhandisi Jackison Mtavanga na Katibu Tawala Msaidizi upande wa maji mkoa wa Dodoma Mathayo Athuman wakipata maelekezo toka kwa Mhandisi Tarcisius Opta ya mita ya malipo ya kabla ya matumizi ya maji 


Wadau wa maji wakiwa katika picha ya pamoja walipokuwa kwenye kongamano la mwaka lililofanyika mjini Dodoma

Mkutano ukiendelea katika ukumbi wa Saint Gasper mjini Dodoma
                                                         Na John Banda, Dodoma

Shirika lisilo la kiserikali la ICS linalojishuhulisha na miradi ya maji vijijini na kwenye mji midogo inayokua, limeanzisha mfumo wa malipo ya kabla ya kupatiwa huduma ya maji ambao utaziwezesha mamlaka za maji kujiendesha, tofauti na ule wa sasa wa kulipia baada ya kutumia ambao umewafanya watu, taasisi na mashirika binafsi na ya kiserikali kukatiwa huduma hiyo kutokana na kulimbikiza madeni.
Akiongea mjini Dodoma Meneja Mauzo wa Taasisi isiyo ya kiserikali ya ICS yenye makao makuu yake Nchini Uholanzi Abraham Mwanyamaki amesema miradi mingi ya maji imekuwa ikifa kutokana na kushindwa kujiendesha kunakosababishwa na madeni ambapo amesema mfumo huo wa malipo ya kabla utawezesha kupatikana fedha zitakazosaidia uendeshaji huo.
Aidha amesema  wananchi wa Maganzo wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga wataanza kufaidika kutokana na  Mradi wa Maji wenye thamani ya zaidi ya 750,mil. uatarajiwa kukamilika mwezi Desemba mwaka huu ambapo kwa kipindi cha miezi 27 tangu umeanza tayari wameshaweka matanki 2 yenye ujazo wa lita 215,000 na kwamba mabomba yatasambazwa mita 200 toka kila nyumba.


Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG