Kwenye interview niliyofanya na Diamond hivi karibuni, nilimuuliza kuhusu kuandamwa na tetesi za kumsaliti mchumba wake Zari na jinsi anavyozichukulia. Katika moja ya majibu yake, staa huyo alisema, “There is no way simba akapita katika zizi la swala akaondoka watu wakasema hakula swala hata mmoja, watasema tu alikula hata kama hakula.”
Na sasa maneno yake huenda yakawa yametimia. Ni kwasababu, Simba anasingiziwa kula swala mzuuuuri wa Zimbabwe, jina lake wa kuitwa Jackie Ngarande.