BANDA MEDIA BLOG

MKURUGENZI WA MANISPAA YA DODOMA AWAPOZA WAFANYABIASHARA JAMATINI

Mkurugenzi wa manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi akizungumza na wafanyabiashara waliyopo kituo cha Daladala jamatini, Stand ya Mabasi na Sarafina alipofika jana kutoa ufafanuzi kuhusu alama za kutakiwa waondoe mabanda yao kwa wiki moja

Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma akimuangalia mfanyabiashara wa viazi akiviondoa baada ya kutakiwa kufanya hivyo kutokana na kufanyia biashara yake mita 2 toka barabara kuu katika eneo la jamatini

Mkurugenzi huyo akiongea na mama muuza matunda katika eneo hilo

mmoja wa wafanyabiashara katika kituo cha daladala jamatini akifafanua jambo wakati alipokuwa akiuliza swali kwa mkurugenzi wa manispaa kuhusu kutakiwa kusaini mkataba wa pili yaani wa Manispaa na Rahco
Na RAMADHAN HASSAN
-DODOMA

SINTOFAHAMU imewakumba  wafanyabiashara katika  stendi za Jamatini,Mkoa na eneo la Sarafina  licha ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma kuahidi kuwa atawasimamia ili waendelea kufanya biashara hadi watakapotafutiwa eneo mbadala.
Sintofahamu hiyo imekuja baada ya Uongozi wa Kampuni hodhi ya mali za Railway (Rahco) kutaka  wafanyabiashara wa maeneo hayo waondoke kwa madai ya kutaka kuanzisha ujenzi wa reli ya standard geji.
Kutokana na hali hiyo jana Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi, alifika katika maeneo hayo na kuzungumza na wafanyabiashara huku akiwasihi kutulia wakati serikali ikiendelea kulifanyia kazi suala lao.
Kunambi alisema tayari alishafikisha kilio chake kwa Rahco na uongozi wa mkoa ili Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) waende kuwaonyesha mipaka halisi ya eneo hilo na kutambua wangapi wako ndani ya eneo la Rahco na wangapi watakuwa chini ya Manispaa.
 “Najua kuwa mnasumbuliwa, lakini naomba tupeane siku saba hapa ili kusudi tuweze kufanya kazi vizuri, Mkuu wa mkoa ameamua kutukutanisha sisi Manispaa, CDA na wenzetu wa Rahco ili kwa pamoja tuweze kuzungumzia jambo hilo, hivyo vuteni subira,” alisema Kunambi.
Awali mwenyekiti wa soko la Jamatini John Banda alisema wafanyabiashara wa maeneo hayo wamekuwa na hali ya sintofahamu kwani Rahco ilishatishia kuwabomolea vibanda vyao pamoja na kuwataka wasaini mikataba kwa haraka.
Banda alisema Rahco wamewapa mikataba wafanyabiashara ili waisaini kabla ya Desemba 31 na wasipofanya hivyo wahesabu wamejiondoa na huenda wakaondolewa kwa nguvu.
Mfanyabiashara Mwajuma Issa alisema shida wanayoipata katika maeneo hayo ni kwa sababu Manispaa ya Dodoma ipo kama nchi inayoelea angani kwa kukosa ardhi chini.
Mwajuma alibainisha kuwa kama Manispaa ingekuwa na ardhi yake bila ya kuingiliwa na CDA huenda mambo yote hayo yasingelitokea kwa wakati huu kwani mpango ungewekwa mahususi kwa ajili kuwasaidia wafanyabiashara.
mwisho

 

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG