BANDA MEDIA BLOG

NAIBU WAZIRI WA NCHI OFISI YA RAIS TAMISEMI SULEMAN JAFFO AWATAKA KUTOPEANA KAZI KIURAFIKI ILI KULETA UFANISI KATIKA MIRADI YA UJENZI


Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa( OR-TAMISEMI) Mhe. Suleimani Jafo  akimpa  maelekezo   Mhandisi  Nelson Maganga   kuhusu   ujenzi wa   madarasa mawili,nyumba za walimu (six in one) ,na matundu 8 ya vyoo  uliopo chini ya mradi wa Secondary Education Development Program  katika  Kata ya Manzase Alhmashauri ya Chamwino wakati alipofanya ziara kujionea maendeleo wa mradi huo mjini Dodoma.

 Picha ikionesha maendeleo ya  ujenzi wa Madarasa Mawili na nyumba za walimu (six in one) ambao upo chini ya  mradi wa Secondary Education  Development  Program (SEDP)  katika kata ya  Manzase ,Alhmashauri ya  Chamwino .


 Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo  akiambatana na watumishi wa Alhmashauri kukagua   maendeleo ya  ujenzi wa madarasa ,nyumba za walimu na matundu ya choo  uliopo chini ya mradi wa  Secondary Education Development Program (SEDP)    katika kata ya Manzase   alipofanya ziara kukagua  maendeleo ya mradi huo  Leo tarehe 13,Desemba ,2016 katika kata hiyo.



Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa( OR-TAMISEMI) Mhe. Seleman Jafo akipokea taarifa za maendeleo ya ujenzi madarasa mawili,nyumba za walimu( six in one), matundu nane ya vyoo, uliopo chini ya mradi wa Secondary Education Development Program (SEDP) kutoka kwa Mhandisi( Ujenzi)  wa Alhmashauri ya Chamwino   Bw. Nelson  Maganga    wakati alipofanya ziara ya kukagua ujenzi  huo unaofanywa katika kata ya Manzase mjini Dodoma aliyoifanya leo tarehe 13 Desemba, 2016. 


 Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo  akikagua  maendeleo ya  ujenzi wa tanki la  maji  katika kata ya Manzase   alipofanya ziara kukagua  maendeleo ya mradi wa maji   Leo tarehe 13,Desemba ,2016 katika kata  ya Manzase , Alhmashauri ya Chamwino .

 Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo  akikagua  maendeleo ya  ujenzi wa tanki la  maji  katika kata ya Manzase   alipofanya ziara kukagua  maendeleo ya mradi wa maji   Leo tarehe 13,Desemba ,2016 katika kata  ya Manzase , Alhmashauri ya Chamwino 
Na Shani Amanzi,
Naibu Waziri Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI)   Mhe. Suleiman Jafo amewataka wahandisi wa mradi wa maji katika kata ya Manzase pamoja na mradi wa ujenzi wa shule ya sekondari ya Manzase uwe ushakamilika na kuacha kupeana kazi kwa mazoea ya kiurafiki.
Naibu Waziri Mhe. Suleiman Jafo  amefanya ukaguzi wa mradi wa maji na ujenzi mapema leo tarehe 13/12/2016, katika kata ya Manzase wilayani Chamwino,mkoani Dodoma na kutolizika na hali iliyokuwepo ya ujenzi katika shule ya  sekondari ya Manzase ambapo walipaswa kukamilisha ujenzi wa madarasa mawili, (six in one) nyumba za walimu na vyoo vya matundu nane.
Mhe. Suleiman Jafo amesema kumekuwa na uchelewaji wa ujenzi kutokana na kukosekana kwa mafundi katika eneo la ujenzi kwa wakati, na kuongeza kwa kusema’’kama  leo wanakamilisha matatizo madogomadogo ya kiufundi na bado hayajakamilika  inaonesha wazi muhandisi wa ujenzi wa shule aliyokabidhiwa kujenga hana uongozi mzuri kwani majengo yangekuwa yashakamilika, na inawezekana kazi mmegawana kirafiki, haiwezekani apewe kazi zote za ujenzi katika maeneo tofauti pasipo kukamilisha ujenzi mmojawapo kwa wakati’’.
Aidha Mhe.Jafo hakufurahishwa pia na ubora wa majengo ya nyumba za walimu kutokana na kuwa na dosari za kuta ikiwemo kupinda na kusema ’’mkurugenzi paka tarehe 20/12/2016 haya majengo yawe yamekamilika na kama hayajakamilika ni marufuku  muhandisi wa ujenzi wa shule hii kupewa kazi ya serikali  popote katika halmashauri ya mkoa wa Dodoma.
Pia  Mhe. Jafo amemtaka  mhandisi wa wilaya ya Chamwino  Bw. Nelson Maganga kupitia mkataba vizuri wa kifedha ikiwa watu wanalipwa vizuri , kwani fedha zipo hapakutakiwa kuwe na dosari yoyote katika ujenzi , na paka tarehe 25-26/12/2016 kazi ya ujenzi iwe imekabidhiwa na kuwataka wahandisi siku nyingine wawe  makini na mafundi  kwani ucheweleshaji wa kazi uwepo kama fedha hawajalipwa
Vilevile Mhe. Jafo alikagua mradi wa maji unaojengwa katika kata ya Manzase na kusema wataalamu wanapaswa kujiongeza ikiwa wananchi wanapata shida ya maji ,wanatembea paka usiku kutafuta maji ,na kumtaka diwani wa kata ya Manzase Mhe. Peter Madanya kuendelea kufatilia kwa karibu zaidi ujenzi wa mradi huo na ifikapo jumatano ijayo atoe taarifa kama hali siyo nzuri kutokana na diwani huyo kusumbuliwa na wananchi juu  ya mradi wa maji umefikia wapi kutokana na kuwa na kero ya muda mrefu  ya tatizo la maji.
Mhe.Jafo ameongeza kwa kusema ’’kwa vile fedha zipo mradi usipokamilika mtoe taarifa jumatano ijayo  na haiwezekani mbunge, diwani na wananchi wanapiga kelele juu ya maji  na mradi haujakamilika , na nataka siku maalum nije kufungua huu mradi  wa maji paka  February 10/2017 ntakuja kufungua huu mradi wa  maji rasmi, na January /2017 nataka hii kazi iwe imekamilika na wananchi waanze kutumia maji ya majaribio.’’

  










Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG