| Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo akikagua maendeleo ya ujenzi wa tanki la maji katika kata ya Manzase alipofanya ziara kukagua maendeleo ya mradi wa maji Leo tarehe 13,Desemba ,2016 katika kata ya Manzase , Alhmashauri ya Chamwino
Na Shani Amanzi,
Naibu Waziri Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) Mhe. Suleiman Jafo amewataka wahandisi wa mradi wa maji katika kata ya Manzase pamoja na mradi wa ujenzi wa shule ya sekondari ya Manzase uwe ushakamilika na kuacha kupeana kazi kwa mazoea ya kiurafiki.
Naibu Waziri Mhe. Suleiman Jafo amefanya ukaguzi wa mradi wa maji na ujenzi mapema leo tarehe 13/12/2016, katika kata ya Manzase wilayani Chamwino,mkoani Dodoma na kutolizika na hali iliyokuwepo ya ujenzi katika shule ya sekondari ya Manzase ambapo walipaswa kukamilisha ujenzi wa madarasa mawili, (six in one) nyumba za walimu na vyoo vya matundu nane.
Mhe. Suleiman Jafo amesema kumekuwa na uchelewaji wa ujenzi kutokana na kukosekana kwa mafundi katika eneo la ujenzi kwa wakati, na kuongeza kwa kusema’’kama leo wanakamilisha matatizo madogomadogo ya kiufundi na bado hayajakamilika inaonesha wazi muhandisi wa ujenzi wa shule aliyokabidhiwa kujenga hana uongozi mzuri kwani majengo yangekuwa yashakamilika, na inawezekana kazi mmegawana kirafiki, haiwezekani apewe kazi zote za ujenzi katika maeneo tofauti pasipo kukamilisha ujenzi mmojawapo kwa wakati’’.
Aidha Mhe.Jafo hakufurahishwa pia na ubora wa majengo ya nyumba za walimu kutokana na kuwa na dosari za kuta ikiwemo kupinda na kusema ’’mkurugenzi paka tarehe 20/12/2016 haya majengo yawe yamekamilika na kama hayajakamilika ni marufuku muhandisi wa ujenzi wa shule hii kupewa kazi ya serikali popote katika halmashauri ya mkoa wa Dodoma.
Pia Mhe. Jafo amemtaka mhandisi wa wilaya ya Chamwino Bw. Nelson Maganga kupitia mkataba vizuri wa kifedha ikiwa watu wanalipwa vizuri , kwani fedha zipo hapakutakiwa kuwe na dosari yoyote katika ujenzi , na paka tarehe 25-26/12/2016 kazi ya ujenzi iwe imekabidhiwa na kuwataka wahandisi siku nyingine wawe makini na mafundi kwani ucheweleshaji wa kazi uwepo kama fedha hawajalipwa
Vilevile Mhe. Jafo alikagua mradi wa maji unaojengwa katika kata ya Manzase na kusema wataalamu wanapaswa kujiongeza ikiwa wananchi wanapata shida ya maji ,wanatembea paka usiku kutafuta maji ,na kumtaka diwani wa kata ya Manzase Mhe. Peter Madanya kuendelea kufatilia kwa karibu zaidi ujenzi wa mradi huo na ifikapo jumatano ijayo atoe taarifa kama hali siyo nzuri kutokana na diwani huyo kusumbuliwa na wananchi juu ya mradi wa maji umefikia wapi kutokana na kuwa na kero ya muda mrefu ya tatizo la maji.
Mhe.Jafo ameongeza kwa kusema ’’kwa vile fedha zipo mradi usipokamilika mtoe taarifa jumatano ijayo na haiwezekani mbunge, diwani na wananchi wanapiga kelele juu ya maji na mradi haujakamilika , na nataka siku maalum nije kufungua huu mradi wa maji paka February 10/2017 ntakuja kufungua huu mradi wa maji rasmi, na January /2017 nataka hii kazi iwe imekamilika na wananchi waanze kutumia maji ya majaribio.’’
|