Michuano ya Mapinduzi Cup
inayofanyika visiwani Zanzibar imefunguliwa jana usiku kwa mahasimu wa
jadi Taifa Jang’ombe na Taifa Boys mchezo uliopigwa kwenye uwanja wa
Aman,Zanzibar huku Taifa Jang’ombe wakiibuka na ushindi wa bao 1-0.
Mshambuliaji Seif Hassan
‘Banda’amekuwa mchezaji wa kwanza kufungua acounti ya magoli katika
michuano hiyo baada ya kuifungia Taifa Jang’ombe dakika za jioni 84
Mpira ulikuwa wa kona ndipo ikiwa piga ni kupige na kumkuta mfungaji
akiwa kwenye nafasi nzuri.
Mechi hiyo ilikuwa na upinzani
mkubwa kutokana na timu zote kutoka mtaa mmoja hivyo kukamiana na
kutambiana nje na ndani ya uwanja kulisababisha mechi hiyo kuwa ya
upinzani mkali.
Kwa matokeo hayo Taifa Jang’ombe
inaongoza kundi A ikiwa na alama tatu mkononi huku ikiwa na timu za URA
toka Uganda ambao ni mabingwa watetezi pamoja na wekundu wa msimbazi
Simba ya jijini Dar es salaam.
Baada ya mchezo huo, Kesho
(Jumamosi) hakutakuwa na mechi, Jumapili ratiba ya Mapinduzi itaendelea
lakini mechi inayosubiriwa kwa hamu ni kati ya Taifa Jangombe dhidi ya
Simba SC ambayo inatarajiwa kuwasili Zanzibar kesho (Jumapili).
Tags
MICHEZO KITAIFA