BANDA MEDIA BLOG

YANGA YANG’ANG’ANIA KILELENI,YALIPA KISASI KWA STAND UNITED


v-Stand
Na.Alex Mathias
Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara Yanga wamelipa kisasi cha paka mwizi kwa wapiga debe toka Shinyanga timu ya Stand United ambao wamekubali kichapo cha magoli 4-0 Mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam
.
Donaldo Dombo Ngoma alifunga bao dakika ya 17 akipokea pasi ya Simon Msuva na kuukwamisha Mpira nyavuni kwa kichwa na dakika ya 26 Simon Msuva aliifungia Yanga bao la pili akimalizia pasi ya Ngoma.
Licha ya kufungwa magoli hayo mawili Stand United hawakukata tamaa kwani mnamo dakika ya 36 Selembe alimanusura aifungie bao timu yake baada ya kuwachanganya mabeki wa Yanga hadi Mapumziko wenyeji walikuwa mbele kwa magoli hayo mawili.
Kipindi cha pili kilipoanza tu Obrey Chirwa aliwanyanyua tena mashabiki wa Yanga dakika ya 45 akifunga bao la tatu baada ya kumpiga chenga Mlinda Mlango wa Stand United na dakika ya 58 Simon Msuva alikosa Penati baada ya kupiga shuti la juu.
Dakika ya 68 Nahodha Nadir Harub ‘Canavaro’ alipigilia Msumari wa nne baada ya kuunganisha Mpira wa Kona iliyochongwa na Simon Msuva hadi dakika 90 zinamalizika Yanga wameibuka na ushindi wa jumla ya magoli 4-0.
Kwa matokeo hayo Yanga wamefikisha pointi 49 na kuendelea kukaa kileleni mwa Ligi Kuu ya Vodacom na nafasi ya pili ikishikwa na Simba wenye pointi 45 ambao kesho nao watakuwa ugenini mkoani Ruvuma kucheza na Majimaji

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG