Mfanyabiashara na muagizaji wa pombe za viroba, Festo Mselia, amekutwa
amejiua kwa kujipiga risasi ikiwa ni siku moja baada ya jeshi la polisi
kuendesha msako na kukamata shehena ya pombe katika ghala alililokuwa
akilimiki mjini Dodoma.
Katika vita ya kupambana na matumizi ya pombe za vifungashio aina ya
viroba vilivyopigwa marufuku, jeshi la polisi mkoa wa Dodoma
limefanikiwa kukamata shehena hiyo ya katoni 1,400 ikiwa na thamani ya
shilingi bilioni moja katika ghala la mfanyabiashara huyo.
Mfanyabiashara huyo aliyejiua ni wakala mkuu wa uagizaji na usambazaji
wa pombe hizo akiwa anamiliki 'store' ya Mselia Intapreses.
Awali katika msako huo ulioongozwa na kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma,
Lazaro Mambosasa, alimtaka mfanyabiashara huyo kuendelea na shughuli
zake, huku akiamuru shehena hiyo isiuzwe wala kutumika wakati akisubiri
maelekezo mengine.
Mambosasa amesema jeshi linaendelea na uchunguzi kabla ua kutoa taarifa rasmi.
Tags
POMBE ZA VIROBA
