Aliyekuwa Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Nape Nnauye leo
amekabidhi ofisi kwa Waziri Mpya wa Wizara hiyo, Dk Harrison Mwakyembe.
Makabidhiano hayo yalifanyika katika Ofisi za Wizara Mjini Dodoma na
kushuhudiwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Profesa Elisante Ole Gabriel.
