Aisee wakuu muwe mna waheshimu sana mama zenu kwa kweli ,kwa niliyoyaona
wodi ya wazazi aiseee nimeathirika kisaikolojia sitamani tena kumtia
mimba mke wangu nahisi kama atakufa kwa kweli.
Roho ilikuwa juu juu kipindi mke wangu anaenda kujifungua ,nilivyoingia
wodi ya wazazi ndio kabisa nikaishiwa nguvu kwa kuwaonea huruma.
Jamani jamani wanawake wanateseka sana wakiwa wanajifungua yani nilihisi mke wangu hatoki akiwa hai lazima afe.
Kwa kweli hata nikipita mtaani minions mwanamke ana ujauzito natamani
kulia kwa kumuonea huruma ,Sitamani kabisa kumpa mke wangu mimba kama
kungekuwa na uwezekano wa kufunga kizazi kwa mwanaume ningeenda walai
Maana wanawake wanapitia mateso makubwa sana.
Ushauri wenu wakuu niondokane na hii hali .
Tags
MIMBA
