BANDA MEDIA BLOG

MAADHIMISHO YA SIKU YA USTAWI WA JAMII DUNIANI MACHI 21


JANM
TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAADHIMISHO YA SIKU YA USTAWI WA JAMII DUNIANI (WORLD SOCIAL WORK DAY) TAREHE 21 MACHI 2017
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa kushirikiana na Chama Cha Wanataaluma ya Ustawi wa Jamii Tanzania (TASWO) inautaarifu umma kuwa itaungana na wataalam wa ustawi wa jamii duniani kote kuadhimisha Siku ya Ustawi wa Jamii Duniani mnamo tarehe 21/03/ 2017 katika viwanja vya Taasisi ya Ustawi wa Jamii iliyoko Kijitonyama, jijini Dar es Salaam kuanzia saa 3.00 asubuhi.

Maadhimisho yatatanguliwa na matembezi ya amani yenye kusisitiza umma juu ya majukumu, wajibu na mchango wa taaluma ya ustawi wa jamii na taifa kwa ujumla. Matembezi hayo yataanzia katika kituo cha mabasi cha ITV kilichopo eneo la mwenge. Mgeni Rasmi katika maadhimisho haya atakuwa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Mb) Mheshimiwa Dkt. Hamis A. Kigwangala.
Kauli mbiu ya siku hii kwa mwaka 2017 inasema “USTAWI WA JAMII: KUKUZA NA KUIMARISHA JAMII NA MAZINGIRA”.
Katika kuadhimisha siku hii huduma za ushauri nasaha, ushauri na upimaji wa Virusi vya UKIMWI, upimaji wa magonjwa ya moyo na huduma nyingine zinazohusiana na matatizo mbalimbali ya kijamii vitatolewa bure. Hivyo, wote mnakaribishwa.
Ili kufikia azma ya serikali ya kuwa nchi ya viwanda, tunahitaji jamii zilizo bora na mazingira rafiki kwa kila mtu hivyo tunatoa rai kwa kila mtanzania kulinda mazingira yanayomzunguka.
Erasto Ching’oro
Msemaji – Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG