BANDA MEDIA BLOG

TATIZO LA AJIRA KWA MADAKTARI KUPUNGUA NCHINI


ke13
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli  na Waziri wa Afya kutoka nchini Kenya Dkt. Cleopa Mailu wakimsikiliza Waziri wa Afya Ummy Mwalimu wakati akizungumza kuhusu Kutangaza ajira za Madaktari wapatao 500 ambao watakwenda kufanya kazi nchini Kenya. Ajira hizo zitawahusu Madaktari ambao hawajaajiriwa Serikalini(hawapo katika utumishi wa umma au taasisi za serikali. PICHA NA IKULU

…………………………………………………………………………………
Na. Immaculate Makilika na Jovina Bujulu-MAELEZO
Dar es Salaam.
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekubali ombi la Serikali ya Kenya la kuwapatia madaktari 500 kufuatia upugufu wa madaktari uliotokana na mgomo nchini humo.
Akizungumza  leo  na waandishi wa habari jijini Dar es salaam, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu alisema kutoka na maombi yaliyotolewa, serikali imeandaa utaratibu kwa madaktari wa kitanzania kuwasilisha maombi yao katika tovuti ya wizara ya afya pamoja kufuata taratibu zingine kama watakavyoelekezwa.
Alizitaja sifa za anayetakiwa  kuomba nafasi hiyo kuwa ni shahada ya kwanza ya udaktari,  mafunzo ya vitendo pamoja na kusajiliwa na Baraza  madaktari la Tanganyika na  kutuma maombi hayo katika barua pepe; maombiyakazi@moh.go.tz  kabla ya Machi 27saa  10 jioni.
Aidha, waombaji wanatakiwa kuambatanisha wasifu wao, nakala za vyeti vya taaluma na  matokeo, cheti cha kuzaliwa, cheti cha kuhitimu mafunzo kwa vitendo pamoja na cheti cha usajili  kutoka Baraza  madaktari la Tanganyika.
“Tanzania hatuna upungufu wa madaktari isipokuwa Serikali haina uwezo wa kuajiri madaktari wote wanaohitimu, kwa kuwa kwa mwaka kuna wahimu 1200 wa shahada ya kwanza ya udaktari na uwezo wa kuajiri ni 450 tu” alisema Ummy
Hata hivyo, Waziri Ummy alisema kuwa ajira hizo hazitawahusu watumishi wa umma, hospitali teule za halmashauri na mashirika ya hiari ambao wanalipwa mshahara na serikali. Madaktari watakaokidhi vigezo na sifa watapewa mkataba wa ajira wa miaka miwili.
Nchi ya Kenya inakabiliwa na upungufu wa madaktari kutokana na mgomo ulioanza mwezi Desemba mwaka jana, ambapo madaktari hao wamekuwa wakaidai nyongeza ya mshahara na marupurupu mengine.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG