Hapa
ni katika ukumbi wa Jensen Complex Hotel uliopo Kakola katika
halmashauri ya Msalala wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga ambapo usiku wa
Machi 08,2017 ,wanawake wanaofanya kazi mgodi wa dhahabu wa Acacia
Bulyanhulu wamefanya hafla fupi ili kusherehekea siku ya wanawake
duniani ambayo hufanyika kila mwaka tarehe 8 mwezi Machi.
Hafla hiyo imeambatana na utoaji
zawadi kwa wanawake wanne shupavu mgodini lakini pia wanawake wote
wanaofanya kazi mgodini wamepatiwa zawadi mbalimbali na Meneja Mkuu wa
Mgodi wa Acacia Bulyanhulu,Graham Crew katika kuadhimisha siku ya
wanawake duniani.
Awali kabla ya kufanya hafla
hiyo,wanawake hao walitoa zawadi ya shuka 140 kwa ajili ya kusaidia
huduma za afya kwa akina mama katika vituo vya afya Bugarama na Lunguya
ambapo pia walitoa zawadi ya sabuni,mafuta ya kujipaka na dawa za meno.
Wanawake hao wametumia fursa
hiyo kuwataka wanawake wengine kujitokeza kufanya kazi katika migodi
badala ya kuamini kuwa kazi za migodini ni kwa ajili ya wanaume tu.
Naye Meneja Mkuu wa Mgodi wa
Acacia Bulyanhulu,Graham Crew alisema mgodi huo hivi sasa unafanya
jitihada za kuwahamasisha akina mama kufanya kazi mgodini ili
kuhakikisha kuwa wanafikia usawa wa kijinsia yaani 50 kwa 50.
Crew aliongeza kuwa hivi sasa wanawake wanashika nyadhifa za juu za uongozi hali inayoonesha wazi kuwa mgodi unajali wanawake.
Mwandishi mkuu wa Malunde1 blog,Kadama Malunde alikuwepo wakati wa hafla hiyo ametusogezea picha 43….Tazama hapa chini
Machi 8,2017 usiku-Mtaalamu wa Mawasiliano mgodi wa dhahabu wa Acacia Bulyanhulu,Mary Lupamba akimkaribisha Meneja mkuu wa mgodi huo Graham Crew
Meneja Mkuu wa mgodi wa dhahabu
wa Acacia Bulyanhulu Graham Crew akizungumza na wafanyakazi wanawake
katika mgodi huo ambapo alisema hivi sasa wafanyakazi wanawake ni
wachache sana ukilinganisha na idadi ya wanaume na kuongeza kuwa mgodi
unafanya jitihada za kuhakikisha kuwa idadi ya wanawake inaongezeka ili
kuwe na usawa wa 50 kwa 50 kwa wanaume na wanawake
Wafanyakazi wa mgodi wa Bulyanhulu wakipiga makofi wakati wakimsikiliza meneja mkuu wa mgodi huo
Meneja Mkuu wa mgodi wa dhahabu
wa Acacia Bulyanhulu Graham Crew alisisitiza pia kuhusu umuhimu wa
kuhamasisha elimu kwa watoto wa kike katika shule za msingi na sekondari
kwani elimu ndiyo itaweza kubadilisha maisha yao
Wanawake wanaofanya kazi mgodi wa Bulyanhulu wakifurahia jambo
Meneja Mkuu wa mgodi wa dhahabu
wa Acacia Bulyanhulu Graham Crew (kushoto) akiteta jambo na Meneja wa
Ustawi wa Jamii na Kampuni ya Acacia Bulyanhulu,Elias Kasitila
Mjumbe wa serikali ya kijiji cha
Kakola kata ya Kakola bi Apaikunda Nathan Palanjo akizungumza wakati wa
maadhimisho hayo ya siku ya wanawake duniani ambapo aliushukuru mgodi
huo kwa kuwasaidia akina mama katika vituo vya afya na kuwasaidia
baiskeli wanafunzi wa shule ya sekondari Bugarama na Bulyanhulu
Meneja Mkuu wa mgodi wa Acacia
Bulyanhulu Graham Crew (wa pili kulia) akiwa ameshikana mkono na
viongozi mbalimbali kuonesha ishara ya umoja wakati wa maadhimisho hayo
ya siku ya wanawake duniani.Wa kwanza kulia ni Meneja wa Ustawi wa Jamii
na Kampuni ya Acacia Bulyanhulu,Elias Kasitila.Wa kwanza kushoto ni
Meneja wa Usalama Acacia Bulyanhulu Terry Little akifuatiwa na mwalimu
mkuu wa shule ya msingi Bulyanhulu ‘A’,Joyce Lwanji na Mjumbe wa
serikali ya kijiji cha Kakola kata ya Kakola bi Apaikunda Nathan Palanjo
Wafanyakazi wa mgodi wa Acacia Bulyanhulu wakiwa wameshikana mkono kuonesha ishara ya umoja
Wafanyakazi wa mgodi wa Acacia Bulyanhulu wakicheza ukumbini
Wanawake wanaofanya kazi katika
mgodi wa Acacia Bulyanhulu wakicheza muziki ukumbini.Kulia ni Mkuu wa
Kitengo cha Mahusiano ya Jamii mgodi wa Acacia Bulyanhulu Sarah Ezra
Terry
Afisa Mahusiano wa Mgodi wa
Acacia Bulyanhulu Zuwena Senkondo akizungumza ukumbini namna
walivyoshiriki katika siku ya wanawake duniani kwa kutembelea vituo vya
afya Bugarama na Lunguya na kutoa zawadi ya baiskeli katika shule ya
sekondari Bulyanhulu na Bugarama
Meneja mkuu wa Mgodi wa Acacia
Bulyanhulu Graham Crew( katikati) akijiandaa kukabidhi zawadi kwa
wanawake wanne shupavu katika mgodi huo ambapo walipewa zawadi ya picha
na shilingi 100,000/= kila mmoja
Meneja mkuu wa Mgodi wa Acacia
Bulyanhulu Graham Crew akikabidhi zawadi ya picha kwa bi Sivirina baada
ya kuonesha utendaji mzuri zaidi kutoka kitengo cha Mazingira.
Meneja mkuu wa Mgodi wa Acacia
Bulyanhulu Graham Crew akikabidhi zawadi ya picha kwa mkuu wa Kitengo
cha Mahusiano ya Jamii mgodi wa Bulyanhulu Sarah Ezra Terry
Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano ya
Jamii mgodi wa Acacia Bulyanhulu Sarah Ezra Terry ambaye anashikilia
nafasi ya juu katika uongozi akipokea zawadi ya picha
Meneja mkuu wa Mgodi wa Acacia
Bulyanhulu Graham Crew akikabidhi zawadi ya picha kwa mwanamke mdogo
kiumri Mwanaisha Moshi ambaye ameonekana kuwa mchapakazi zaidi
Meneja mkuu wa Mgodi wa Acacia
Bulyanhulu Graham Crew na Meneja wa Ustawi wa Jamii na Kampuni ya Acacia
Bulyanhulu,Elias Kasitila wakiwa wamejifunga mitandio ya akina mama
baada ya kuwavalisha mitandio wanawake wanaofanya kazi mgodini kama
sehemu ya zawadi ya meneja mkuu wa mgodi huo
Wanawake wanaofanya kazi mgodini
wakiwa wamevaa mitandio waliyozawadiwa na Meneja mkuu wa Mgodi wa
Acacia Bulyanhulu Graham Crew
Meneja wa Ustawi wa Jamii na Kampuni ya Acacia Bulyanhulu,Elias Kasitila akicheza muziki na wanawake wanaofanya kazi mgodini
Meneja mkuu wa Mgodi wa Acacia Bulyanhulu Graham Crew akiangalia wafanyakazi wa mgodi huo wanavyocheza muziki
Muziki unaendelea
Mtaalamu wa Mawasiliano mgodi wa dhahabu wa Acacia Bulyanhulu,Mary Lupamba akicheza muziki
Muziki unaendelea
Akina mama wakicheza muziki
Meneja wa Usalama Acacia
Bulyanhulu Terry Little akicheza muziki na Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano
ya Jamii mgodi wa Acacia Bulyanhulu Sarah Ezra Terry
Muziki umekolea……
Muziki umenoga haswaaa….
Kushoto ni Maria na Sarah wakifungua shampen
Maria na Sarah wanafungua shampen
Maria na Sarah wameshafungua shampen
Wafanyakazi wa mgodi wa Acacia Bulyanhulu wakigonga cheers
Mjumbe wa serikali ya kijiji cha
Kakola kata ya Kakola bi Apaikunda Nathan Palanjo akigonga cheers na
Meneja wa Ustawi wa Jamii na Kampuni ya Acacia Bulyanhulu,Elias
Kasitila.
Zoezi la kugonga cheers linaendelea
Cheers!!!!
Meneja mkuu wa mgodi wa Acacia Bulyanhulu Graham Crew akigonga cheers na wafanyakazi wake
Meneja wa Usalama mgodi wa Acacia Bulyanhulu Terry Little akigonga cheers na wanawake wanaofanya kazi mgodini
Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano ya Jamii mgodi wa Bulyanhulu Sarah Ezra Terry akiwa na furaha ukumbini
Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano ya
Jamii mgodi wa Bulyanhulu Sarah Ezra Terry na Meneja mkuu wa Mgodi wa
Acacia Bulyanhulu Graham Crew
Picha ukumbini
Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano ya
Jamii mgodi wa Bulyanhulu Sarah Ezra Terry akiwaasa wafanyakazi wenzake
kufanya kazi kwa juhudi huku akieleza kuwa wanawake wana nafasi kubwa
ya kushika uongozi mgodini
Kushoto ni Afisa Mahusiano wa Mgodi wa Acacia Bulyanhulu Zuwena Senkondo akibadilishana mawazo na wafanya kazi wenzake.
Picha zote na Kadama Malunde-Malunde1 blog
<<<Picha>>>WANAWAKE
MGODI WA BULYANHULU WASHEREHEKEA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI KWA KUTOA
MSAADA KWA WANAFUNZI NA WAGONJWA
Tags
WANAWAKE