Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,
Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) George Simbachawene
akizungumza na wafanyabiashara wa Soko la Machinga Complex alipofanya
ziara kwa ajili ya kusikiliza changamoto zao leo Jijini Dar es Salaam.
Kutoka Kushoto ni Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam Sipora Liana,
Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam Theresia Mmbando, Mkuu wa Mkoa wa
Dar es Salaam Paul Makonda na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema.
Mmoja wa wafanyabiashara
katika Soko la Machinga Complex akielezea changamoto wanazokumbana nazo
katika soko hilo mbele ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Tawala za
Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) George Simbachawene (hayupo
pichani) alipotembelea katika soko hilo leo Jijini Dar es Salaam. Waziri
Simbachawene amefanya ziara katika Soko hilo hili kusikiliza changamoto
kutoka kwa wafanyabiashara hao na kukagua utekelezaji wa agizo
alilolitao wakati wa ziara yake ya kwanza sokoni hapo mapema mwaka jana.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,
Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) George Simbachawene
(wapili kutoka kushoto) akitembelea baadhi ya vizimba vya wafanyabiasha
katika soko la wafanyabiashara wadogowadogo la Machinga Complex leo
Jijini Dar es Salaam. Kutoka Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam
Paul Makonda, Meneja wa Soko hilo, na Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es
Salaam Theresia Mmbando.
Na: Mpiga Picha Wetu.
………………
Na: Frank Shija – MAELEZO, Dar es Salaam.
WAFANYABIASHARA ndogondogo katika
Soko la Machinga Complex Jijini Dar es Salaam wameshauriwa kubadilika na
kuendesha shughuli zao kwa kuzingatia sheria badala ya kufanya biashara
zao kimazoea.
Wito huo umetolewa leo na Waziri
wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
George Simbachawene alipofanyaa ziara ya kikazi katika Soko hilo ili
kusikiliza changamoto wanazokumbana nazo wafanyabiashara wa soko hilo.
“Nawapa pole sana ndugu zangu
wafanyabiashara wa Machinga Complex mnaendesha biashara zenu bila
kuzingatia sheria jambo linalo wagharimu hivi sasa katika biashara zenu
leo nimekuja kuwarejesha kwenye mstari,” alisema Simbachawene.
Aidha Waziri Simbachawene
amemuagiza Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam kuwachukulia hatua baadhi
ya viongozi wa menejimenti ya Machinga Complex kwa kile kinachodaiwa
utendaji wao mbovu na kujaza nadfasi zote zilizo wazi,
Wakati huohuo amemwagiza Mkuu wa
Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda kuteua Wajumbe wa Bodi ya Machinga
Complex ili kuongeza ufanisi katika uendeshaji wa Soko hilo.
Pia Waziri Simbachawene ametoa
wito kwa wafanyabiashara wote kulipa kodi zao kwa wakati huku hakitishia
kuwaondoa katika vizimba (eneo la mraba la mauzo) wale wote watakao
kaidi amri hiyo halali ya kulipa kodi kwa mujibu wa sheria na mikataba
yao.
Awali akimkaribisha Waziri
Simbachawene, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amesema kuwa
ujio wa Waziri huyo mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa imekuja wakati
muafaka kwani ni takribani kipindi cha karibu mwaka mmoja tangu alipompa
maagizo ya kushughulikia changamoto zinazokabili jengo la Machinga
Complex kazi ambayo waliikamilisha na kukabidhi taarifa katika ofisi ya
Waziri Simbachawene.
“Nidhahiri kuwa ziara yako Mhe.
Waziri itatoa majawabu yatakayopelekea kutatua changamoto kadhaa
zinazolikabili soko hili la Machinga Complex na ni imani yangu kwamba
utatoa maagizo na kufanya maamuzi nasi hatuna budi ya kuyapokea na
kutekeleza” alisisitiza Makonda.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Jiji
la Dar es Salaam Bibi. Sipora Liana amesema kuwa changamoto kubwa
inayokabili Soko hilo ni pamoja na deni linalokadiriwa kufikia zaidi ya
shilingi bilioni 38 zianzodaiwa na Shirika la hifsdhi za Jamii (NSSF)
ambao ndiyo waliojengwa majengo ya soko hilo linalomilikiwa na
Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam.
Aliongeza kuwa changamoto nyingine
inayokabili Soko hilo ni kutokuwapo kwa chombo cha maamuzi (Bodi)
ambayo kazi yake kubwa ingekuwa kushughulikia changamoto zote za mradi
huo.
Soko la Machinga Complex
limejengwa kwa lengo la kutatua changamoto ya ukosekanaji wa soko la
uhakika kwa wafanyabiashara wadogowadogo katika Jiji la Dar es Salaam
ambapo ujenzi wake ulifanyika chini ya udhamini wa NSSF na kumilikiwa na
Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam likiwa na uwezo wa kuchukua
takribani wafanyabiashara 4206.
Tags
MACHINGA