BANDA MEDIA BLOG

YANGA YATUPWA NJE LIGI YA MABINGWA AFRIKA,SASA KUCHEZA KOMBE LA SHIRIKISHO


YANGA NA ZANACO
Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara timu ya Yanga  imengukia tena kwenye Kombe la Shirikisho Afrika baada ya kutolewa katika michuano ya Ligi ya Mabingwa baada ya sare ya 0-0 na Zanaco FC kwenye uwanja wa Taifa wa Mashujaa uliopo mjini Lusaka Zambia.

Matokeo hayo yanamaanisha Yanga inatolewa kwa bao la ugenini, baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 kwenye mchezo wa kwanza wiki iliyopita Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. 
Kwa Mpaka mwamuzi toka Kenya anapuliza kipyenga cha mwisho timu hizo zinametoshana nguvu na kwa matokeo hayo Zanaco FC wametinga hatua ya Makundi na wanajangwani hao itabidi wasubiri droo ya kombe la Shirikisho ili kujua wanakutana na nani na kuweza kutafuta nafsi ya kuingia hatua ya makundi ikumbukwe mwaka jana walitolewa na Al-Ahly Ligi ya Mabingwa na kudondokea Shirikisho ambapo walitenga hatua ya Makundi

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG