Wananchi wa nchi ya Uturuki wamemaliza kupiga kura ya maoni ambayo
ilikuwa iamue kama Katiba ya nchi hiyo ibadilishwe na kumpa Raisi wa
nchi madaraka makubwa kama ya Raisi wa JMTZ au ibakie kama ilivyo na
madaraka madogo ambayo yako limited!
Sasa matokeo ya kura ya maoni yameonyesha kwamba wengi wao wanapendelea
kuwa na Kiongozi mwenye madaraka makubwa yaani strongman dhidi ya Katiba
ambayo madaraka ya Raisi yamevunjwa vunjwa kama waliyo nayo leo hii,
matokeao ni 51.39% Ndiyo, na waliobakia Hapana!
Na tayari Raisi wa USA Donald Trump amempigia simu Raisi Tayyip Erdogan
na kumpongeza kwa ushindi huo, sasa Uturuki inaongozwa na Katiba ambayo
inampa Raisi madaraka makubwa sana!
Raisi Tayyip Erdogan sasa ni strongman wa nchi ya Uturuki!
Tags
uturuki
